• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Jiji la DSM kufanya kazi kikanda

Posted on: July 19th, 2023

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo Tarehe 19 Julai, 2023 imetoa taarifa kwa Umma na wadau kwa ujumla kupitia vyombo vya habari kuwa,imegawanya eneo la Jiji katika kanda za kiutawala ili kurahisisha utoaji wa huduma unaolenga kutoa huduma zenye ubora na usawa kwa jamii kwa kuzingatia utawala bora na kutumia kikamilifu rasilimali zilizopo.

Akitoa taarifa hiyo katika ukumbi wa mikutano wa Arnatoglou uliopo Mnazi Mmoja Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bi.Tabu Shaibu amesema kuwa kuanzishwa kwa huduma za Kanda kutaongeza wigo wa ukusanyaji wa Mapato kwa kuwa ufuatiliaji wa walipa kodi utafanyika kwa ukaribu na ufanisi na kuiwezesha Halmashauri kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Vilevile amesema kuwa kutasaidia kuweka mipango itakayozingatia mahitaji maalum ya maeneo tofauti kwa kuwa kila eneo linaweza kuwa na changamoto na mahitaji yake ya kipekee ,kugawa maeneo kutawezesha kubuni na kutekeleza programu zitakazozingatia mahitaji ya kila eneo.

Aidha ameongeza kuwa mpango huu utarahisisha ufanisi na usimamizi wa utoaji huduma kwa kuwa na eneo dogo ambapo kutasaidia kuimarisha usimamizi wa huduma za Umma na kusababisha utendaji kazi ulio bora na uwezo wa kurekebisha kwa haraka changamoto zinazojitokeza hivyo kuimarisha utekelezaji mzuri wa bajeti na mipango ya maendeleo.

Amesema, “Kuwepo kwa kanda kutasaidia kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za wananchi kwa wakati kwa kuwa wakati mwingine matatizo ya wananchi yanashindwa kutatuliwa kwa wakati kwa sababu ya umbali wa kuzifikia huduma wanazozihitaji”

Bi. Tabu amesema kuwa kutakuwa na jumla ya Kanda 7 za kutolea huduma ambapo Kanda namba 1 ina Kata za Kivukoni, Kisutu, Upanga Mashariki na Upanga Magharibi na Ofisi ya Kanda itakuwa katika ofisi ya Kata Upanga Mashariki.

Kanda namba 2 ina Kata za Ilala, Mchikichini, Jangwani, Kariakoo, Gerezani na Mchafukoge, Ofisi ya Kanda itakuwa katika ofisi ya Kata Gerezani.

Kanda namba 3 inahusisha Kata za Buguruni, Mnyamani, Vingunguti, Kipawa, Minazi Mirefu na Kiwalani. Ofisi ya Kanda itakuwa katika Ofisi ya Kata ya Mnyamani .

Kanda namba 4 itajumuisha Kata za Tabata, Liwiti, Kimanga, Kisukulu, Segerea, Bonyokwa na Kinyerezi. Ofisi ya Kanda itakua katika Ofisi ya Kata ya Kinyerezi.

Kanda namba 5 itakuwa na Kata za Ukonga, Gongo la Mboto, Pugu Stesheni na Pugu na Ofisi ya Kanda hii itakuwa katika Ofisi ya Kata ya Gongo la Mboto.

Kanda namba 6 ina Kata za Kitunda, Mzinga, Kivule, Kipunguni na Majohe ambapo wananchi wa Kata hizi watahudumiwa katika Ofisi ya Kata ya Kipunguni.

Kanda namba 7 inahusisha kata za Buyuni, Chanika, Zingiziwa na Msongola ambapo Ofisi ya Kata ya Chanika itatumika kama Ofisi ya Kanda hii.

Vituo hivi vya kanda tayari vimekwishaanza kutoa huduma chini ya Uongozi wa Mameneja wa Kanda.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.