• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii Jiji la DSM yafanya Ziara ya ukaguzi wa Miradi ya Afya

Posted on: April 30th, 2024

Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo Aprili 30, 2024 imefanya ziara ya ukaguzi wa Miradi ya Afya lengo likiwa ni kufuatilia utekelezaji wa shughuli za kimaendeleo zilizotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kipindi cha robo ya tatu kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kilichoanza Januari hadi Machi 2024.

Ziara hiyo ililenga kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya Afya inayoendelea kutekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kujionea maendeleo ya miradi hiyo jinsi  itakavyorahisisha huduma mbalimabali za afya kwa Jamii pindi itakapokamilika.

Aidha, Miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa jengo la kuhifadhia maiti katika Kituo cha Afya Chanika uliogharimu kiasi cha shilingi milioni 107 ujenzi ukiwa katika hatua ya umaliziaji, ujenzi wa jengo la mionzi (X-Ray) Kituo cha Afya Pugu uliogharimu kiasi cha shilingi milioni 107 utekelezaji wa mradi ukiwa hatua ya ukamilishaji pamoja na uwekaji mashine ya mionzi huku ujenzi wa ghorofa 5 Kituo cha Afya Mchikichini ukiwa umekamilika kwa asilimia 40 ambapo sakafu mbili zimekamilika na sakafu ya tatu imeanza kujengwa.

Akizungumza katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mheshimiwa Saady Khimji amesema kuwa “Leo tumetembelea baadhi ya Miradi ya Afya inayosimamiwa na kutekelezwa na Halmashauri ya Jiji la DSM ambapo tumeweza kuridhishwa na utekelezaji huo hivyo nitoe wito kwa Watendaji wa Halmashauri kusimamia miradi hii kwa ukaribu zaidi na Sisi kama wasimamizi tutaendelea kushirikiana nao kuhakikisha miradi hii inatekelezwa kwa wakati na thamani ya Fedha inayotumika inalingana na ubora wa miradi kwani Kamati hufanya ziara hizi kwa lengo la kukagua na kuhakikisha fedha zinazotolewa na Serikali Kuu pamoja na Halmashauri zinawafikia walengwa na kufanya kazi kama ambavyo fedha hizo zimeelekeza.  Hivyo naomba mapungufu yaliyoonekana kwenye miradi hii yashughulikiwe kwa wakati ili wananchi wote wafikiwe na huduma muhimu na bora kwa wakati kama Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavyoonesha juhudi zake katika kuwahudumia Wananchi.”

Sambamba na hilo Mhe. Khimji ameendelea kusema ni wajibu wa kila Mtendaji kuhakikisha anasimamia vyema shughuli za maendeleo ili kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuleta maendeleo ya pamoja kwa Jamii

“Sera ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa wakati kwani sisi kama wasimamizi hatutavumilia watu wanaokwamisha kwa makusudi miradi ya maendeleo hivyo nipende kutoa wito kwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es salaam kuhakikisha anashirikiana na watendaji wake kwa ukaribu kusimamia miradi hii ya afya ikamilike kwa wakati uliopangwa lengo ni kuwasaidia wananchi wetu kupata huduma bora kwa wakati. Pia tusisahau kuwashirikisha wananchi katika kufanikisha miradi kwani miradi hii inawalenga wao moja kwa moja." Amesisitiza Mhe. Khimji.

Aidha, Wajumbe wa Kamati wameridhia kuwa endapo kutakua na changamoto wakati wa utekelezaji wa miradi ni vyema changamoto hizo zikawasilishwa sehemu husika mapema na kufanyiwa kazi ili maendeleo ya wananchi yasikwamishwe huku wakiagiza wahandisi kutoka Halmashauri kuhakikisha wanasimamia kwa ukaribu zaidi ujenzi wa Miradi ya Maendeleo ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na iwe yenye ubora.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.