• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Lishe Bora Ni Muhimu kwa Ukuaji wa watoto Kimwili na Kiakili

Posted on: April 4th, 2023

Serikali ya Tanzania imedhamiria kuendelea kulipa umuhimu wa kipekee suala la lishe nchini ili kuhakikisha Tanzania inakuwa na uchumi imara kupitia maendeleo ya viwanda. “Maendeleo ya Taifa pamoja na mambo mengine, yanahitaji uwepo wa watu (nguvu kazi) wenye afya njema na lishe bora ili kuwawezesha kufanya kazi kwa bidii na Kuchochea maendeleo ya nchi."

Katika kutekeleza hilo leo Aprili 04, 2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia kitengo cha Afya na Lishe wameendelea kutoa elimu ya lishe kwa wananchi wa Kata ya Buguruni ikiwa ni sehemu ya kutekeleza mpango wa kutoa elimu ya lishe kwa watoto katika Kata 36 na Mitaa 159 ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kipindi cha robo ya mwaka 2022/2023.

Aidha katika hafla hiyo wataalamu waliweza kupima hali ya lishe kwa watoto kuanzia miez 6 hadi miaka mitano lengo likiwa ni nikujua hali ya Afya ya watoto na kwa wale watakabainika kuadhirika na utapiamlo watapata rufaa ya kwenda kupata huduma katika kituo cha Afya anapoishi.

Akitoa mafunzo hayo ya lishe Afisa Lishe wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Neema Mwakasege amesema “Lishe bora ni kula chakula cha kutosha na chakula chenye virutubisho vyote muhimu. Lishe bora husaidia mwili kukua vyema, kuujenga mwili lakini pia huimarisha kinga ya mwili ili kuweza kupigana na magonjwa. Ili lishe iwe bora ni muhimu iwe na mchanganyiko wa Makundi sita ya chakula ambayo ni protini, wanga, fati, mbogamboga, madini, matunda na maji kwa wingi hivyo tuhakikishe tunawapa watoto mlo kamili lengo likiwa ni kupunguza udumavu na kuongeza uelewa kwa watoto wetu kwani lishe bora ndio msingi wa makuzi ya kimwili kwa watoto hawa.

Hata kama tunaanda mlo kamili tusipoandaa kwenye mazingira safi itakua ni kazi bure hivyo inabidi tuhakikishe tunaandaa vyakula hivyo katika mazingira, tunahifadhi chakula sehemu safi na salama pamoja na kuchemsha maji ya kunywa ili tukinge afya za watoto wasiadhiriwe na magonjwa nyemelezi”. Amesema Bi. Mwakasege 

Sambamba na hilo Bi. Mwakasege amewahimiza wazazi/walezi kuhakikisha wanawapeleka watoto kliniki hadi watakapofikisha miaka 5 ili kuweza kujua hali zao huku akiwataka wazazi/walezi ambao watoto wao hawajapata chanjo ya Surua wahakikishwe wanawapeleka kituo cha afya kupata chanjo hiyo ili wasije wakalemaa.

Kwa upande mwingine Afisa Ustawi kutoka Kituo cha Afya Buguruni Bi. Sophia Elias Kadonge amewataka wazazi/walezi kuhakikisha wanakata bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa ambayo inatumika kuanzia ngazi ya zahanati kituo cha afya mpaka hospitali za rufaa za Mkoa kama Hospitali ya Amana hivyo amewahimiza wazazi/walezi kukata bima ya afya iliyoboreshwa ili iweze kuwasaidia katika matibabu pindi mtu anapopata matatizo ya kiafya.

Sambamba na hilo Bi. Sophia Elias Kadoke amewataka wazazi/walezi kuwalinda watoto zidi ya ukatili wa kijinsia kwani janga hili linaonekana kuchukua nafasi kubwa sana katika Jamii zetu kwa sababu ya kukosa elimu ya namna ya kujikinga na matatizo haya hivyo amewaasa endapo mzazi/mlezi ataona dalili za ukatili au mtoto anafanyiwa ukatili ni vyema kutoa taarifa kwa maafisa ustawi ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.