• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Miradi ya Shilingi Bilioni 46.8 yatembelewa na Mwenge Maalum wa Uhuru Wilaya ya Ilala

Posted on: August 19th, 2021

Na: Hashim Jumbe 

"Sisi tumekwisha uwasha Mwenge, tumekwisha uwasha Mwenge. Na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro. Kuwasha Mwenge na kuuweka Kilimanjaro" 

Naam, huo ni mpangilio wa sauti za kizalendo zilizobeba maudhui ya wimbo wa kuwashwa kwa Mwenge wa Uhuru, sauti kutoka kwa Vijana wa Halaiki wa Wilaya ya Ilala, ziliposikika asubuhi ya leo ya Tarehe 18 Agosti, 2021 kwenye viwanja vya ndege vya Dar es Salaam (terminal one) zikiashiria kuwa Mwenge wa Uhuru umewasili ndani ya viunga vya Wilaya ya Ilala

Aidha, wakati wa makabidhiano ya Mwenge huo wa Uhuru, Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa, Luteni Mwambashi alisisitiza kuwepo kwa nyaraka na vielelezo vyote muhimu kwenye miradi ya Mwenge watakayoitembelea, huku Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija akieleza kwa ufupi miradi watakayotembelea na kuifanyia ukaguzi pamoja na kuweka mawe ya msingi "katika Wilaya ya Ilala, Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru mwaka 2021 zitapitia jumla ya miradi ya maendeleo 9 yenye jumla ya thamani ya Shilingi Bilioni 46.8"

Miradi iliyotembelewa kwa Wilaya ya Ilala ni pamoja na miradi Miwili (2) ya Vikundi vya uzalishaji mali vya vijana ambapo miradi hii imewezeshwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia  mkopo wa asilimia 10% ya mapato ya ndani pamoja na kituo cha Mifumo ya TEHAMA 'Buguruni'

Mradi mwingine ni uboreshaji wa miundombinu ya ujenzi wa barabara ya lami, Stendi ya Kinyerezi na daraja la Ulongoni B ambao umewekwa jiwe la msingi, Mradi wa ujenzi wa madarasa ya ghorofa Shule ya Sekondari Ilala-Kasulu, mradi wa ujenzi wa kituo cha Polisi Mzinga ambao umetekelezwa kwa nguvu ya Wananchi na wenyewe umewekewa jiwe la msingi.

Vilevile mradi wa afya wa wadau ambao ni ujenzi wa Hospitali binafsi ya AL-AMAL uliopo chini ya Asasi ya Direct Aid Society (DAS) inayojulikana kwa jina la Africa Muslims Agency na wenyewe umewekewa jiwe la msingi na mradi wa utengenezaji wa samani za chuma wa kikundi cha DAGE cha Watu wenye Ulemavu kutoka kata ya Vingunguti ambao umewezeshwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia  mkopo wa asilimia 10% ya mapato ya ndani, mradi huu umetembelewa na kukaguliwa na pia mbio za Mwenge zilikagua mradi wa mwaka 2019 kuona maendeleo yake,  mradi huo ni ujenzi wa Tanki la kuhifadhia maji lita Milioni 2 lililopo Pugu

Aidha, wakati akitoa Salamu na Ujumbe wa Mwenge wa Uhuru 2021 kwa Wananchi wa Wilaya ya Ilala, Kiongozi wa Mbio za Mwenge, Luteni Josephine Paul Mwambashi, Mwambashi alielezea mambo muhimu likiwemo la matumizi ya malipo ya kietroniki katika ukusanyaji wa mapato kwa ngazi ya Halmashauri, huku akiwaasa Wananchi kutokufanya malipo bila ya kupewa risiti ya EFD kwani kutokuchukua risiti kunaipunguzia Serikali mapato, lakini pia alisisitiza juu ya madhara ya madawa ya kulevya, huku akihimiza matumizi ya lishe bora ili kujenga jamii imara na kuendelea kujikinga na maambukizi ya virusi vya UKIMWI ili kuikinga jamii yetu.

Mbio za Mwenge wa Uhuru 2021 zimebeba ujumbe unaosisitiza matumizi ya TEHAMA katika kuchochea maendeleo "TEHAMA ni Msingi wa Taifa Endelevu, Itumike kwa Usahihi na Uwajibikaji".

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.