• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Awataka Wananchi Kupanda Miti Kwa Wingi

Posted on: March 29th, 2023

Katika kuelekea Siku ya Upandaji Miti ambayo hufanyika Kitaifa kila tarehe 01, Aprili, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Jonas Mpogolo leo Machi 29, 2023 amefanya kikao na waandishi wa habari lengo likiwa ni kuhabarisha, kuelimisha na kuhamasisha Umma juu ya upandaji wa miti hasa katika kipindi hichi cha mvua.

Akizungumza katika Kikao hicho Mhe. Mpogolo amesema ”Lengo la mkutano huu ni kuhabarisha, kuelimisha na kuhamasisha wananchi wa Wilaya ya Ilala kupanda miti kwa wingi hasa kipindi hichi cha mvua kwani kauli mbiu ya mwaka huu katika siku ya mazingira ni ‘Misitu ni Afya’ hivyo kutokana na kauli mbiu hii Inabidi tupande miti kwa wingi kwa afya na kwa kukuza uchumi pia, Sisi kama Wilaya tumedhamiria kupanda miti Takribani milioni 1.5 kama alivyoelekeza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philp Isdori Mpango mnamo Novemba 2022 akiwa Mbeya kuwa kila Halmashauri wahakikishe wanapanda miti takribani milioni 1.5 hivyo sisi tunatekeleza hilo ambapo kwa mwaka 2022 tuliweza kupanda takribani miti milioni 1.3 hivyo na mwaka 2023 tutahakikisha tunapanda miti milioni 1.5 katika baadhi ya maeneo yetu mabalimbali”.

Aidha Mhe. Mpogolo ameeleza kuwa kutokana na Kauli mbiu ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akishirikiana pamoja na Mkuu wa Mkoa ya ‘Mti wangu’ Wilaya ya Ilala watahamasisha zoezi la upandaji miti katika Shule za Msingi na Sekondari ambazo zina takribani wanafunzi laki 4 ambapo kila mwanafunzi akipanda mti wake zoezi hilo litakua limekamilika kwa kiasi kikubwa.

vilevile Mhe. Mpogolo amewataka viongozi wa Serikali za Mitaa na Kata kuhakikisha wanawahimiza wananchi wao kupanda miti kwa wingi huku akiwataka watu wenye majengo pembezoni mwa barabara pamoja na viwanda kuhakikisha wanapanda miti kwenye vungu na kuviweka mbele ya majengo yao ili kupendezesha mazingira na kuvutia mandhari ya Jiji letu la Dar es Salaam ambalo ndio kitovu cha wageni wengi wanapoingia Nchini Tanzania.

Sambamba na hilo Mhe. Mpogolo ameeleza kuwa kwa upande wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam itapanda miti ya matunda pamoja na miti ya kivuli hususani maeneo ya Mashuleni, pembezoni mwa barabara zetu na miti mingine itapandwa pembezoni mwa bonde la mto Msimbazi  "Kwa upande wetu Jiji la Dar es Salaam tutashirikiana na Wenzetu wa TFS kwani wameahidi kushirikiana na sisi katika kupendezeshanmazingira yetu hivyo wameahidi kutupatia miche ya miti mbalimbali inayoweza kupandwa katika Jiji letu.”

Aidha Mhe. Mpogolo ametoa wito kwa Wananchi kuhakikisha wanapanda miti kwa wingi kwani sheria ya saivi inamtaka mwananchi atenge asilimia 5 ya ardhi yake kuwa kijani hivyo ametaka Idara ya Mazingira ya Jiji la Dar es Salaam kuhakikisha wana kitalu cha miti kwani wataalamu wapo ambao watasaidiana nao kukamilisha jambo hilo la kupendezesha mazingira .

Kwa upande mwingine Mhe. Mpogolo alihitimisha kwa kuwataka wananchi kuchukua tahadhari kipindi hichi cha mvua hasa wanapovuka katika maeneo ya mito huku akitoa maagizo kwa Viongozi wa Serikali za Mitaa na Kata kuhakikisha wanachukua hatua za kisheria kwa wananchi wote wanaotiririsha maji taka wakati wa mvua hivyo kwa wananchi wote waliounganisha mfumo wa maji taka na mfumo wa maji ya mvua wahakikishe wanaacha tabia hiyo kwani wanachafua mazingira.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.