• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

RC DSM Azindua Mkakati endelevu wa Usafi na Uhifadhi wa Mazingira

Posted on: November 22nd, 2021

Na. Judith Damas

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amezindua mkakati endelevu wa Usafi na uhifadhi wa mazingira Dar es salaam ambapo ameelekeza kila Mtendaji kusimamia Usafi na kuhakikisha sheria inatumika kutoa adhabu kwa wachafuzi wa mazingira, hayo ameyabainisha leo Novemba, 23 katika mkutano wa Uzinduzi wa Usafi na uhifadhi wa Mazingira Dar es Salaam  wenye kauli mbiu isemayo 'Safisha Pendezesha Dar es Salaam' uliofanyika katika  Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, ukiwa umehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa kiserikali, Chama Cha Mapinduzi, Viongozi wa Dini, Wastahiki Meya, Vyombo vya ulinzi na usalama, Maafisa Mazingira, Wenyeviti na Watendaji wa Mitaa na wadau mbalimbali.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe.  Makalla ametoa maelekezo 10 kwa Viongozi wote na wananchi wazingatie  ili kufanikisha Kampeni hiyo ikiwemo Kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kuwa siku ya Usafi wa pamoja "Kila Manispaa iteue wakandarasi wa Usafi Wenye Sifa na Vigezo, ikiwemo Vifaa vya kutosha vya kufanyia Usafi, Kila Manispaa kupitia upya Sheria za udhibiti wa Biashara holela na Usafi na Kama hazipo zitungwe, Kila Mwenyekiti na Mtendaji wa Mtaa kuhamasisha na kusimamia Usafi kwenye eneo lake, Mkataba na kila Manispaa kusimamia Usafi na Machinga wasirudi kwenye maeneo yaliyokatazwa, kila Taasisi kulinda maeneo yake  ili yasivamiwe na Machinga, Wakuu wa Wilaya kusimamia Usafi katika maeneo ya fukwe zote za Mkoa huo kufanyiwa Usafi na uwe endelevu, Amepiga marufuku tabia ya Wizi wa vyuma na minyororo iliyowekwa kwaajili ya kupendezesha mandhari ya Jiji(vigingi) pia ameeleza kuwa usafi unaendana na muonekano mzuri wa majengo hivyo ameelekeza majengo yote yapakwe rangi yawe na muonekano mzuri.

Sambamba na hayo Mhe. Makalla ametoa wito kwa Wananchi kuitumia siku ya tarehe 4 Desemba ambayo ndiyo siku ya  uzinduzi wa Usafi Kata ya Kivukoni kwa kufanya Usafi wa kina kwenye maeneo yao ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Sherehe za Uhuru.

Kwa upande Mwingine Mhe. Makalla ameweza kuingia mkataba na Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi wote wa Kila Halmashauri kusimamia usafi na Kuhakikisha Wafanya biashara ndogondogo hawarudi tena katika maeneo yasiyo rasmi na maeneo hayo yafanyiwe usafi wa kina.

"Mkataba huu ulioambatana na mahudhurio kama makubaliano ya kutekeleza suala zima la usafi na uhifadhi wa mazingira utasainiwa na Mkuu wa Wilaya pamoja na Mkurugenzi wa kila Halmashauri na mkitoka hapa mhakikishe mnapitia sheria ndogondogo za usafi na kama hazipo mkazitunge, muende mkajifunze kwa wenzenu waliwezaje kufanikisha suala zima la usafi Katika Mikoa yao." Ameeleza Mhe. Makalla.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa DSM Bi. Cathe Kamba amempongeza Mkuu wa Mkoa wa DSM pamoja na Viongozi wake kwa kazi nzuri walioifanya ya kuwapanga wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Machinga kutoka sehemu zisizo rasmi na kwenda kufanya biashara maeneo rasmi hivyo ameahidi kushirikiana na viongozi hao katika kampeni ya usafi na uhifadhi wa mazingira Mkoa wa Dar es Salaam na kuhakikisha Mkoa unakua safi.

Akitoa shukrani zake Kwa Mkuu wa Mkoa Mwenyekiti wa Machinga  Bw. Masoud Issa amesema" Tunamshukuru Mkoa wa Mkoa Mhe. Makalla kwa kutushirikisha katika zoezi zima la kutupanga katika maeneo rasmi na kwaniaba ya Wamachinga wenzangu naahidi hatutomuangusha tutabaki katika maeneo rasmi na tutahakikisha tunafanya usafi na  tunahifadhi mazingira ili kuipendezesha Dar es Salaam."

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.