• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

RC Makonda aweka jiwe la Msingi la Mradi wa Viwanda Vidogo Vidogo vya Wajasiriamali

Posted on: September 9th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Paul C. Makonda leo tarehe 09 Septemba, 2017 ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa viwanda vidogo vidogo vinavyojengwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam katika eneo la Mwananyamala jijini Dar es Salaam ili kuwawezesha wajasiriamali kuboresha ustawi wa maisha yao.

Akiongea katika hafla hiyo Mhe. Makonda ametoa pongezi kwa Waheshimiwa Madiwani na watendaji wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kujenga na kuboresha mazingira rafiki kwa lengo la kuchochea maendeleo kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam.

Ameongeza kuwa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi imetaja utaratibu wa kuweka asilimia 10 ya fedha za mapato ya ndani ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa ajili ya Wanawake, Vijana na Walemavu na kuagiza kwamba Manispaa za Jiji la Dar es Salaam ziige mfano wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliyoanza ujenzi wa miundombinu rafiki kwa wanufaika wa mikopo kwa kuhakikisha kwamba inawajengea miundombinu wanufaika wa mikopo ya Halmashauri katika kila Manispaa za Jiji la Dar es Salaam.

Mhe Makonda amesema mfumo wa sasa hauna utambuzi wa kutosha kwa vijana, wanawake na walemavu kutokana na makundi hayo kutawanyika kibiashara jambo linalosababisha changamoto ya ufuatiliaji wa mikopo hiyo, na kuziagiza Manispaa za Jiji la Dar es Salaam kutenga maeneo maalum ya uanzishaji wa VIWANDA VIDOGO VIDOGO kwa ajili ya makundi hayo, hatua itakayowaweka pamoja na hivyo kutoa fursa kwa Serikali ya Mkoa kuwahudumia vizuri hususan katika kuwawezesha kupata mafunzo ya kuwaongezea ujuzi na utaalamu, masoko na pia kuwaunganisha na Wafanyabiashara wakubwa.

Awali akiwasilisha taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bi. Sipora Liana alimweleza Mhe. Paul Makonda kuwa ujenzi wa viwanda hivyo ni sehemu ya utekelezaji wa Kauli Mbiu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli, inayochochea uanzishwaji wa viwanda nchini kufikia malengo ya uchumi wa kati ambapo Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, pamoja na kuwawezesha wawekezaji wakubwa wa viwanda kufikia malengo yao na kuwajengea mazingira bora ya uwekezaji, imepanga kujenga viwanda vidogo vidogo kwa ajili ya akina mama, vijana na walemavu wa Jiji la Dar es Salaam pamoja na kuwapatia fedha za mikopo zinayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

"Katika Mwaka wa Fedha 2016/2017, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ilitenga kiasi cha shilingi 200,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vidogo vidogo ambao utekelezaji wake  ulianza tarehe 01 Juni, 2017 ambapo hadi kufikia mwezi Agosti, 2017 ujenzi wa miundombinu hiyo umefikia asilimia 95. Gharama za mradi huo ni shilingi 199,988,052.00. Ujenzi huo utaendelea kutekelezwa na Halmashauri ya Jiji katika Manispaa za Ilala, Kigamboni, Temeke na Ubungo kwa kadri maeneo yatakavyopatikana", alieleza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji.

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo inashirikiana na Shirika la Kukuza Viwanda Vidogo Vidogo(SIDO) kuwajengea uwezo wajasiriamali hao itawawezesha kupata mafunzo yatakayowasaidia kuboresha zaidi uzalishaji na biashara zao. Kwa upande mwingine itakuwa rahisi zaidi kwao kupata mikopo kutoka kwenye taasisi za fedha, wadau mbalimbali pamoja na huduma muhimu kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA) na wadau wengine.

Kwa kutumia vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya nchi, tovuti ya Halmashauri pamoja na mitandao ya kijami, Halmashauri ya Jiji itawasaidia wajasiriamali hao kujitangaza zaidi ili waweze kupata masoko ya bidhaa zao ndani na nje ya nchi na inatoa wito kwa wajasiriamali wote watakaopata nafasi katika viwanda hivyo kuitunza miundombinu katika maeneo yote yatakayojengwa viwanda hivyo kwa maslahi ya wananchi wote.

Bonyeza hapa kuangalia picha zaidi za tukio hilo.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la Msingi Kituo cha Afya Mzinga

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wakagua mradi wa vijana "Ulipo Tupo" Tabata

    June 03, 2025
  • Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Magengeni - Chang'ombe umewekewa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wazindua mradi wa Nishati Safi Soko la Samaki Feri

    June 03, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.