• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Uzinduzi wa Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii katika Jiji la Dar es Salaam

Posted on: June 30th, 2017

NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Nuru Milao  ameupongeza Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kulitoa jengo la kale la Old Boma ambalo lina zaidi ya miaka 160 liweze kutumika kama Kituo cha Urithi wa Ubunifu wa Majengo na Utalii. 

Jengo la Old Boma lenye historia kubwa katika nchi yetu ambalo limefanyiwa ukarabati kwa kiwango cha juu na kuwa mfano wa uhifadhi endelevu na kituo cha kutangaza historia ya ukuaji wa miji yetu kanda ya Afrika Mashariki kwa ufadhili wa Umoja wa Nchi za Ulaya.

Akizungumza katika hafla ya kufungua kituo hicho leo Jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt.Harrison Mwakyembe (MB), Milao alisema hatua hiyo inadhihirisha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kuwa utamaduni wa Mtanzania unadumishwa na kukuzwa.

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Waheshimiwa Madiwani wa Jiji la Dar es Salaam wakiongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji Isaya Mwita Charles, Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya, Balozi wa Ufaransa, wananchi na wadau mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam.

Mgeni rasmi pia amesifu juhudi zinazofanywa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam za kuvitangaza vivutio vya utalii jijini kwa lengo la kuogeza pato kupitia shughuli za utalii na mipango yake ya kuwa na mabasi ya Halmashauri ya kuhudumia watalii.

Bi. Nuru pia ametoa pongezi kubwa kwa Jumuiya ya Wabunifu Majengo Tanzania na washirika wake kwa juhudi wanazofanya za kuanzisha mpango wa kuelimisha, kutunza na kudumisha majengo ya kale ambayo utakua ukisaidia kukuza na kuendeleza utalii katika Jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.

Akihitimisha hotuba yake mgeni rasmi ametoa wito kwa wananchi na wadau wote kuwa na mawazo ya utunzaji wa majengo ya kale badala ya uvunjwaji wa majengo hayo kama inavyoendelea katika Jiji la Dar es Salaam bila kupata vibali vya mamlaka husika Serikalini.

Mgeni rasmi ametoa msisitizo kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa katika Jiji la Dar es Salaam  wa kusimamia sheria na kushughulikia kero zinazotokana na udhaifu wa kutosimamia sheria ambazo kimsingi zingeweza kusaidia kuimarisha usalama na kutunza mazingira ya majengo yote ya kale na majengo ya kisasa ambayo ni sehemu kubwa ya vivutio vya utalii nchini.

Naye  Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Isaya Mwita Charles ameeleza kuwa kufunguliwa kwa kituo hiko ni fursa ya kukuza pato la uchumi la wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na taifa kwa ujumla kupitia mapato ya watalii watakaokitembelea.

"Tayari tumeweka mipango mbalimbali ya kukuza, kuhifadhi, kutangaza vivutio vya utalii tulivyonavyo na kuvifanya kuwa vyanzo vikubwa vya mapato katika Jiji letu ikiwemo utoaji mafunzo kwa madereva Teksi ambao wanahusika katika kuwasafirisha  watalii ili wawe na uelewa zaidi kuhusu kituo hiki” alisema Mstahiki Meya wa Jiji.

Kwa Upande wake Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya Mhe. Roeland Van De Geer amesema ofisi yake iko tayari kushirikiana kwa karibu na Jiji la Dar es Salaam na Tanzania katika kukuza na kuendeleza majengo ya kale na katika kuleta maendeleo kwa ujumla.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.