• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Vikundi vya Wajasiriamali Ilala vyapewa semina ya mafunzo juu ya umuhimu na matumizi ya mfumo wa Msimbomilia (Barcode)

Posted on: March 9th, 2023

Mkuu wa Wilaya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amewahakikisha Wajasiriamali Wilaya ya Ilala kuwapa ushirikiano pale wanapohitaji ili kukuza Masoko ya Wajasiriamali hao.

Amebainisha hayo leo Machi 09, 2023 wakati akifungua Semina ya Mpango wa Mafunzo ya Ujasiriamali kwa ngazi ya Halmashauri iliyofanyika katika Ukumbi wa Arnatoglou Jijini Dar es Salaam, Semina hiyo iliwezeshwa na taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo TRA, TIRDO, TCCIA, BRELLA, TANTRADE na TBS.

Akifungua mafunzo hayo Mhe.Mpogolo Amesema “Mafunzo haya ni adhimu sana kwa wajasiriamali kwani suku hii ya leo watapata mafunzo haya yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kutafuta Masoko baada ya kuweka bidhaa zao Barcodes ambayo itawasaidia kuuza bidhaa hizo kwenye masoko rasmi hivyo niwaombe Wajasiriamali msikilize kwa makini na muende mkaishi haya yote mnayoelekezwa.”

Kwa upande mwingine Mhe. Mpogolo aliweza kuzindua kampeni ya GS1 Tanzania Barcode day itakayoanza June 15-19, 2023 yenye kauli mbiu isemayo ‘GS1Tanzania beyond Barcode’ ambapo aliweza kuwasisitiza wajasiriamali kujitokeza kwa wingi, “Ili kuwakomboa kina mama lazima kina mama muungane na mimi niwahakikishieni kwenye hiyo kampeni ya Kata kwa Kata nitakuwepo kwani tutafanya kwa niaba ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan ambaye nia yake ni kuwakomboa wananchi kiuchumi hususani Wanawake hivyo nawapongeza GS1 na timu nzima kwa kampeni hizi naamini kila Mjasiriamali wa Wilaya ya Ilala atanufaika na fursa hii.”

Naye Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salam Bi. Tabu Shaibu awashukuru GS1 kuandaa semina ya mafunzo kwa Wajasiriamali ambayo itawasaidia kupata uelewa jinsi ya kuboresha bidhaa zao ili ziwe na viwango na ubora na kuweza kukidhi Soko la ushindani ambapo zitaweza kukuwa na kufikia Soko la kimataifa.

Aidha, kwa upande wake mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Halmshauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Tabu Shaibu amemuhakikishia Mkuu wa Wilya kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Kitengo chake cha Maendeleo ya Jamii iko tayari kuyafanyia kazi yale yote yaliyoelekezwa kwenye semina hiyo ili kuinua Wajasiriamali hao.Pia awataka Wajasiriamali kusikiliza kwa makini semina hiyo ya mafunzo ili kutoka na uelewa jinsi gani ya kuboresha bidhaa zao.

Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa GS1 Bi. Kange Ameeleza kuwa “Baada ya Wajasiriamali kuonekana wanazalisha bidhaa bora lakini hazina msimbomilia(BARCODE) Ofisi ya Rais TAMISEMI wakaona ni vyema kutoa kibali kwa Taasisi ya GS1 ambao ndio hutengeneza Barcodes kuandaa mafunzo katika kila Halmashauri nchini ya kuwafundisha Wajasiriamali umuhimu wa Barcodes ambapo kila Halmshauri iliweza kuingia makubaliano ya mafunzo hayo kwa kuchangia Shilingi Milioni 5 zakuwezesha mafunzo hayo hivyo mafunzo haya ya kuwajengea uwezo Wajasiriamali juu ya umuhimu na matumizi ya msimbomilia (BARCODES) yameanza kufanyika leo kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambapo vikundi Vitano (5) Vitaweza kuchaguliwa."

Sambamba na hilo Bi. Kange ameeleza kuwa baada ya mafunzo wataweza kuwasaidia wafanyabiashara kutafuta masoko kwani kuna masoko Canada na Marekani ila masoko haya yatahudhuriwa na vikundi ambavyo vitaweza kukidhi vigezo na pia vitakavyotengeneza bidhaa bora na zenye viwango

Aidha Bi.Kange ameendelea kusema “Sisi kama wajasiriamali tuhakikishe tunatengeneza bidhaa kwa kiwango na pia tunaweka mifumo kupitia Maafisa Maendeleo wa Halmashauri ya Jijj la Dar es Salaam huku tukipanga kiwango cha pamoja cha kuuza bidhaa zetu hivyo niwasisitize mtengeneze kurasa za mitandao ya kijamii kwaajili ya kutafuta masoko rasmi.”

Vilevile Bi.Kange amshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kufungua mipaka ambayo ni fursa kwa wananchi wa Tanzania, “Naamini sisi kama wajasiriamali tutatumia fursa hii ya mheshimiwa Rais wetu hivyo sisi GS1 tutashirikiana na wajasiriamali kupata masoko nje ya nchi ya Tanzania hivyo tutahakikisha tunawaelekeza namna ya kutengenezea kurasa katika mitandao ya kijamii na namna gani mnaweza kupata masoko.”

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.