• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Wajumbe TSC wahimizwa kusimamia Utumishi na Maadili ya Walimu

Posted on: September 25th, 2024

Wajumbe wa Kamati za Nidhamu za Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania (TSC) kwa ngazi ya Wilaya wamehimizwa kuendelea kutekeleza jukumu la Msingi la kuhakikisha wanasimami Utumishi na Maadili ya Walimu ili kuwa na Walimu wenye kujituma na wanaozingatia maadili ya kazi yao kwaajili ya kuwalea watoto kwa usahihi na kuboresha elimu nchini.

Wito huo umetolewa leo Septemba 25, 2024 na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Zainab Katimba (Mb) wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya wajumbe wa Kamati za nidhamu za Tume ngazi ya Wilaya yanayofanyika katika Ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam kwa Kanda ya Mashariki iliyojumuisha Wilaya za Mikoa ya Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Pwani na Morogoro.

Akiongea wakati wa ufunguzi huo, Mhe. Katimba ameipongeza Tume ya Utumishi wa Walimu pamoja na wajumbe wake kwa utendaji mzuri wa kazi unaoambatana na uzoefu na uaminifu katika kutekeleza Majukumu yao.

"Nipende kutoa pongezi zangu kwa Tume pamoja na wajumbe wa Kamati kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuhakikisha mnateleleza majukumu ya kisheria pamoja na kusimamia utumishi wa Walimu kwani mafunzo haya yana lengo la kuwawezesha wajumbe wa Kamati kufahamu wajibu wao katika kusimamia ajira, nidhamu na maadili ya Walimu hivyo ni imani yangu mafunzo haya yatakua chachu ya kuongeza ufanisi katika kutekeleza majukumu ya Tume na Serikali kwa Ujumla lengo likiwa ni kuendana na kauli mbiu ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhun Hassan ya 'Kazi Iendelee' na Sisi kama viongozi tutaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha ili kazi ziendelee kufanyika kwa ufanisi na uadilifu." Amesisitiza Mhe. Katimba.

Awali akitoa salamu wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu Prof. Masoud Mureke ameeleza kuwa lengo la mafunzo ni kuwajengea uwezo wenyeviti na wajumbe wa Kamati za Tume za Wilaya ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi huku akiahidi kuwa Tume itaendelea kusimamia jukumu lake la msingi la usimamizi wa Utumishi na Maadili ya Walimu kwa lengo la kuhakikisha Walimu hao wanazingatia maadili kwa manuafaa ya watoto na kuendelea kuboresha Elimu Nchini.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Msaidizi wa Tume Wilaya ya Ilala Mwl. Subira Mwakibete ameeleza kuwa baada ya mafunzo hayo yenye lengo la kuwajengee uwezo wajumbe wa Kamati za Tume za Wilaya ni imani kwao wataendelea kutekeleza majukumu yao ipasavyo ili kuhakikisha sekta ya elimu nchini inakua na Walimu wanatimiziwa stahiki zao muhimu kwa wakati.

Aidha, Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku Siku mbili (2) kwa wajumbe wa wilaya 139 kwa Kanda tano (5) ambazo ni Kanda ya Kaskazini ambapo mafunzo yanafanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa Jiji la Arusha kwa Wajumbe wa Wilaya za Mikoa ya Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga, Kanda ya Mashariki ambapo mafunzo yanafanyika katika Ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam kwa Wajumbe wa Wilaya za Mikoa ya Lindi, Mtwara, Dar es Salaam, Pwani na Morogoro, Kanda ya Kati ambapo mafunzo yanafanyika katika Ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora katika Manispaa ya Tabora kwa  Wajumbe wa Wilaya za Mikoa ya Kigoma, Katavi, Tabora, Singida, Tabora na Dodoma, Kanda ya Ziwa ambapo mafunzo yanafanyika katika Ukumbi wa Nyakahoga Jijini Mwanza   kwa Wajumbe wa Wilaya za Mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Geita pamoja na Kanda ya  Nyanda za Juu Kusini ambapo mafunzo yanafanyika katika Ukimbi wa Dkt. Shein Jijini Mbeya kwa Wajumbe wa Wilaya za  Mikoa ya Rukwa, Songwe, Ruvuma, Njombe, Iringa na Mbeya.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.