• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Wanawake wa Mkoa wa DSM wahamasishwa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Posted on: May 22nd, 2024

Wanawake wa Mkoa wa Dar es Salaam wametakiwa kuwa mabalozi katika matumizi ya Nishati Safi na salama ya kupikia,lengo likiwa ni kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za utunzaji wa Mazingira.

Wito huo umetolewa na Mshauri wa Rais katika masuala ya wanawake na makundi maalumu Dkt. Sophia Mjema, wakati wa Mkutano wa Uzinduzi wa Programu ya ‘Imarisha Uchumi na Mama Samia’ (IMASA) iliyofanyika Leo Mei 22, 2024  katika Ukumbi wa Arnatoglou Jijini Dar es Salaam na kuwakutanisha viongozi mbalimbali wa majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi Mkoa wa Dar es Salaam, Taasisi  na Mashirika binafsi.

Aidha, Dkt. Mjema amesema "Lengo la Serikali ni kuhakikisha kila Mkoa, Wilaya, Kata na Mitaa kunakuwa na sehemu ambapo wananchi wataweza kupata nishati Safi na salama ya kupikia kwani kupitia nishati safi tutahakikisha usalama, uendelevu na urahisi wa upatikanaji wa nishati ya kupikia, kuokoa muda, pamoja na kupunguza gharama za matumizi, athari za kimazingira na kiafya kwa watumiaji. Pia, ni nyenzo muhimu katika kutekeleza makubaliano ya kitaifa na kimataifa yanayolenga kupambana na mabadiliko ya tabianchi na kupunguza uzalishaji wa gesi joto”.

Sambamba na hilo, Dkt. Mjema amemshukuru Rais Jamhuri ri ya Muungano wa Tanzania kwa kuja na mkakati wa matumizi safi ya nishati ya kupikia huku akiwashukuru Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa kuja na Programu ya ‘Imarisha Uchumi na Mama Samia’ ambayo itakua chachu ya kuwakutanisha wanawake na wananchi katika kujadili masuala mbalimbali ya Kiuchumi bila kusahau suala la nishati safi ya kupikia.

Awali akiongea wakati wa Mkutano huo Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Toba Nguvila amesema “Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Jamhuri ri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa na maono ya kuwakwamua wananchi kiuchumi kwani Mkoa wa Dar es Salaam uko tayari katika kutekeleza programu hii ya IMASA inayolenga kutambua na kuwezesha shughuli za Kiuchumi na ukizingatia Dar es Salaam ni Mkoa wenye fursa za kiuchumi na uwezeshaji wa wanawake kiuchumi hivyo kuja kwa programu hii katika Mkoa wetu ni fursa kwetu hivyo ninawahakikishia ushirikiano katika kutekeleza mpango huu na nitoe wito kwa wanawake na makundi maalumu  kushiriki kikamilifu katika hili kwani huu ni wakati muafaka kwenu wa kujikwamua kiuchumi”.

Naye, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bi. Bengi Issa ameeleza kuwa  mpango huo unafungua milango kwa wanawake kutambulika rasmi wao na biashara zao na mahali wanapofanyia shughuli zao za kibiashara kwani biashara nyingi ndogondogo za wanawake sio rasmi na wengi hawana leseni hivyo kupitia mpango huu wanawake watawaweza kujikwamua kiuchumi kwani watapatiwa mikopo kwaajili ya kukuza mitaji yao.

“Pamoja na mambo mengine mpango huo utaweza kutengeneza kanzidata ya kupata takwimu za wanawake hapa nchini na hizo ni juhudi za Serikali za kuanzisha programu hii ambayo itasimamiwa na baraza ili kuweza kuwapa elimu kuhusu mambo ya kodi, biashara , ujasiriamali , kanuni na sheria mbalimbali hapa nchini”. amesema Bi. Issa






Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.