• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Watendaji wa Kata, Mitaa pamoja na Wenyeviti wa Mitaa wa Jiji la DSM wakumbushwa kutekeleza majukumu yao kwa Uadilifu

Posted on: June 27th, 2023

Maafisa Watendaji wa Kata, Mitaaa pamoja na Wenyeviti wa Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wametakiwa kufanya kazi ya kuwahudumia wananchi kwa weledi kwa kuzingatia uadilifu na maadili ya Utumishi wa Umma.

Maagizo hayo yametolewa Leo Juni 27, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo wakati wa kikao kazi cha kukumbushana majukumu ya kazi zao, maadili ya utumishi wa umma sambamba na usimamizi wa miradi inayotekelezwa katika Halmashauri kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Shaaban Robert Uliopo Upanga Jijini Dar es Salaam.

Aidha Akiongea katika kikao hicho Mhe. Mpogolo amewataka Watendaji wa Kata, Mitaa pamoja na Wenyeviti wa Mitaa kuhakikisha wanafanya kazi kwa ushirikiano pamoja na kujenga mahusiano mazuri na wananchi, Madiwani pamoja na viongozi wote wa Chama cha Mapinduzi lengo likiwa ni kutekeleza Ilani ya Chama pamoja na kutambua kazi kubwa anayoifanya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha Wananchi wanapata huduma bora kwa ukaribu na uharaka zaidi.

Sambamba na hilo Mhe . Mpogolo amesema “Napenda kuwapongeza wote kwa kazi Nzuri mnazozifanya za kusimamia miradi pamoja na kuhudumia wananchi licha ya changamoto ndogondogo zinazowakabili Ila nipende kuwakumbusha mfanye kazi zenu kwa uadilifu msijihusishe na kazi za ukusanyaji wa mapato kwani sio kazi zenu hivyo mtekeleze majukumu yenu ya kuwahudumia Wananchi kwa ukaribu zaidi ili kutekeleza adhma ya Rais wetu ya kuhakikisha kila Mwananchi anapata huduma bora kwa wakati”.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Ndg. Jomaary Mrisho Satura aliweza kuwapongeza Watendaji pamoja na Wenyeviti kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuwahudumia wananchi katika maeneo yao huku akiwakumbusha kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu hasa kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu na maelekezo maalumu ya Serikali.

“Kikao kazi hichi kina lengo la kuwakumbusha wajibu na majukumu yenu katika kusimamia mapato pamoja na utekelezaji wa miradi kwani imani yangu ni kuwa kila mtu anaomuongozo wa majukumu anayopaswa kutekeleza kila siku, kila mtu anafahamu sheria, kanuni na taratibu za kazi lakini zaidi zingatieni na kutekeleza maagizo yanayoshushwa kwenu, kwa kutoka ofisi ya Mkurugenzi, kwa kutambua kuwa mnaowajibu wa kufanyakazi kwa niaba ya Mkurugenzi katika maeneo yenu." Amesisitiza Ndg. Satura.

Akifunga Kikao hicho Mastahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto amesema “Tumedhamiria kubadilisha Jiji letu hivyo fedha zinapotolewa zitumike kwa uangalifu na kwa uaminifu ili kufikia malengo hivyo tuwe waadilifu katika kusimamia utekelezaji wa miradi yetu pia kwa kushirikiana Mkurugenzi tutahakikisha tunasimamia vyema majukumu yetu ikiwa ni kusimamia vyema utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji letu”.

Hata hivyo Maafisa Watendaji hao, wameushukuru uongozi wa Halmashauri kwa kikao kazi hicho chenye tija na kuahidi kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma ili kufikia malengo ya Serikali ya kuwahudumia wananchi katika maeneo yao.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.