• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Watendaji wa Sekta ya Elimu Jiji la DSM watakiwa kupandisha ufaulu, huku wakisaini mikataba ya uwajibikaji

Posted on: January 16th, 2023

Watumishi wa Idara ya Elimu Msingi na Idara ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo tararehe 16 Januari, 2023 wamefanya kikao kazi cha pamoja katika ukumbi wa Shule ya Msingi Mnazi Mmoja, lengo likiwa ni kuboresha Sekta ya Elimu ili wanafunzi waweze kupata elimu katika mazingira mazuri ambayo yatapelekea kupandisha ufaulu wao.

Kikao hicho kiliwahusisha Walimu Wakuu wa Shule za Msingi za Serikali, Wakuu wa Shule za Sekondari za Serikali, Waratibu wa Elimu Kata na Maafisa Elimu kutoka Idara za Elimu za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, ambapo Mkuu wa Wilaya ya Wilaya Ilala, Mhe. Ludigija alitumia fursa hiyo kuwataka Watendaji katika Sekta ya Elimu kufuata maelekezo yaliyoelekezwa na Serikali ikiwa ni pamoja na mahudhurio, ufundishaji na ufundishwaji kuwa na mikakati na mbinu katika kutekeleza hayo kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha kila mtoto anakuwa Shuleni na kupata matokeo chanya.

Sambamba na hilo lakini pia Mkuu wa Wilaya ameagiza Wakuu wa Shule za Sekondari kuhakikisha Wanafunzi wote waliopangwa Katika Shule zilizopo Wilaya ya Ilala wanaripoti huku akiwapongeza Wakuu wa Shule za Sekondari kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa madarasa “Niwapongeze Wakuu wa Shule za Sekondari kwa usimamizi mzuri wa ujenzi vyumba vya madarasa, kwa kweli mmejitahidi kuendana na kasi na madarasa yamejengwa kwa ubora unaotakiwa” Amesema Mhe. Ludigijja.

Naye, Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mwl. Musa Ally amesema matarajio yao ni kuhakikisha maelekezo yote yaliyotolewa kwenye Vigezo vya Utendaji vinafikiwa kwa Asilimia 100 na kuhakikisha miundombinu katika Sekta ya Elimu kama madarasa, matundu ya vyoo, maabara, mabweni inaimarika.

Vilevile Sekta hiyo ya Elimu imejipanga kuhakikisha ufaulu katika Halmshauri hiyo unapanda kutoka asilimia 35 mpaka asilimia 50 na zaidi, wanafunzi wa Kidato cha Nne kufaulu kwa daraja la Kwanza, Pili na Tatu kwa ufaulu wa A, B, C sambamba na udahili na mahudhurio vifikie asilimia 100.

“Lengo letu ni kufanya yasiyowezekana yawezekane kwa kuhakikisha miundombinu katika Sekta ya Elimu inaimarika na mazingira mazuri yote yanayofanya mwanafunzi kuweza kusoma vizuri yanafanyika” Amesema Mwl. Mussa Ally.

Akizungumza katika Kikao hicho Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mwl. Sipora Tenga amesema kupitia kikao hicho watahakikisha kila Afisa Elimu wa Kata na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam awajue wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika na kuwapeleka katika hatua nzuri kulingana na Kata zao lakini pia watahakikisha Walimu wanaofundisha Darasa la Tatu wanakuwa mahiri katika somo la Kiingereza ili kuwajengea Wanafunzi wa Darasa la Tatu umahiri wa lugha ya kiingereza.

Sambamba na hayo kikao hicho pia kiliambatana na kusaini kwa mkataba wa Uwajibikaji na Utendaji Kazi kwa Maafisa Elimu Kata, Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na Wakuu wa Shule za Sekondari ndani ya Halmshauri hiyo.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.