• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA ILALA KATIKA KATA YA PUGU-GONGO LA MBOTO YATOA NJIA UTATUZI WA CHANGAMOTO YA MAJI.

Posted on: May 26th, 2021

ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA ILALA KATIKA KATA YA PUGU - GONGO LA MBOTO YATOA NJIA UTATUZI WA CHANGAMOTO YA MAJI.

Na Amanzi Kimonjo.

Mkuu wa wilaya ya Ilala Mhe.Ngw’ilabuzu Ndatwa Ludigija tarehe 26 mei 2021 ametembelea mradi wa ujenzi wa tanki na mfumo wa usambazaji wa maji uliopo Pugu-Gongolamboto Jijini Dar Es Salaam tenki ambalo linachukua ujazo wa lita milioni mbili ambalo limeshakamilika kwa asilimia mia moja na zoezi la usambazaji wa maji umeanza kwa kata ya Pugu maeneo ya Buyuni, Majoe, Gongo la mboto, Pugu Stesheni,na sehemu ndogo ya Chanika huku wananchi  wakifurahia huduma ya maji na baadhi yao wako katika utaratibu wa kusambaziwa maji.

Hata hivyo, Mradi huu unaotoa bomba kuu la kusambaza maji lenye urefu wa kilomita 13.5 kutoka Kisarawe mpaka Ukonga Air wing pamoja na tenki lenye ujazo wa lita milioni mbili likiambatanishwa na mabomba madogo yenye upana wa  ‘inch’ tatu hadi nane ya kusambaza maji  katika Kata hizo yakiwa yamekamilika kwa asilimia mia moja.

Aidha, Mkuu wa wilaya Mhe. Ludigija amesema “Natoa pongezi kwa  Mamlaka ya Maji Safi na Salama Dar es Salaam (DAWASA) kwa kuwezesha usimamizi na taratibu za usambazaji wa maji, kubwa zaidi kwa Wilaya ya Ilala ninatamani mradi huu uwe sehemu ya wananchi kupata maji na kuondokana na adha ya maji”. Hivyo tatizo la muda mrefu la ukosefu wa maji kwa kata ya Pugu-Gongolamboto litakua historia baada ya mda mchache.

Vile vile, Msimamizi wa mradi huu Mhandisi Ishumaili Kakwezi amesema “usambazaji wa maji unaendelea kwa mahitaji ya wateja na mpaka sasa tumewafikia wateja 2000 na wengine tunawaungia mabomba lengo huduma hii ya maji iwafikie kwa uharaka”.

Kwa upande mwingine Mkuu wa Wilaya Mhe.Ludigija alitembelea  mradi wa ujenzi wa daraja  la Ulongoni A na Ulongoni B iliyoko chini ya mradi mkubwa wa DMDP ambapo ujenzi wa daraja la Ulongoni A uliogharimu shilingi billion 4.5 umefikia  asilimia 79 na inategemewa kufikia mwezi wa sita wananchi wataanza kutumia daraja hilo,  huku daraja la Ulongoni B lililo gharimu takribani shilingi billion 2.5  ujenzi bado unaendelea.

“Ninamshukuru Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam,  wataalamu wetu wakiongozwa na Mhandisi Magori, Mkandarasi na wengine walioshiriki katika kufanikisha ujenzi huu kwa hatua ulipofikia maana naona matumaini kua ifikapo tarehe 10 mwezi wa sita wananchi wataanza kutumia daraja hili  na inafahamika mradi huu utamalizika tarehe 30 mwezi wa sita na nitoe wito kwa wataalamu wa Jjiji,mkurugenzi,mkandarasi,Tarura, waongeze kasi ya ujenzi huu nafarijika kuona jinsi kazi inavyoendelea  na tutafuatilia mpaka hapo mradi huu utakapo malizika”.

Akitoa shukrani zake kwa viongozi Mhandisi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhandisi .Magori amesema “Mradi huu wa ujenzi wa Daraja la ulongoni unaendelea na kwa niaba ya Halmashauri tunamshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa pesa kuendeleza mradi huu pamoja na  viongozi wetu Wakiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na Katibu tawala wa Wilaya ya Ilala kwa kuonyesha ushirikiano wao wa kutembelea  na kuifatilia miradi hii toka imeanza mpaka hapa ilipofikia”.

Ziara hii  ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala iliweza kumalizika kwa kutembelea ujenzi wa stendi ya Kinyerezi  unaombatana na ujenzi wa barabara kutoka ulongoni B hadi kufika katika stendi  hiyo ya Kinyerezi  ambapo barabara hiyo yenye kilometa 9.5 ikiwa inaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami.

Ukamilifu wa  Stendi hii ya Kinyerezi ambayo ni kitovu  cha biashara na shughuli nyingine za kiuchumi  inategemewa na wananchi wa Kinyerezi pamoja na wananchi wa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Dar es salaam kwani ipo karibu na stendi kuu ya mabasi ya  kwenda mkoani (Stendi ya Magufuli )hivyo basi itarahisisha wananchi wote wa Ilala kuweza kufika na kupata huduma.

Akihitimisha ziara yake  Mkuu wa Wilaya  ya Ilala Mhe. Ludigija amesema “Mkandasi pamoja na wasaidizi wake wasibweteke kwa sifa hizi tunazowapatia bali wafanye kazi na waongeze kasi wasiseme Mkuu wa Wilaya amepita na kazi isimame nataka hadi kufikia tarehe 30, Juni 2021 kazi hii iwe imekamilika kama ilivyokusudiwa.”

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la Msingi Kituo cha Afya Mzinga

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wakagua mradi wa vijana "Ulipo Tupo" Tabata

    June 03, 2025
  • Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Magengeni - Chang'ombe umewekewa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wazindua mradi wa Nishati Safi Soko la Samaki Feri

    June 03, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.