• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Zoezi la upandaji Miti laendelea kwa Kasi Wilaya ya Ilala

Posted on: March 31st, 2023

Katika kuelekea siku ya upandaji miti Kitaifa ambayo hufanyika kila tarehe 1 Aprili Wilaya ya Ilala leo tarehe 31, Machi 2023 wameadhimisha siku ya upandaji miti kwa ngazi ya Wilaya ambapo miti 300 imeweza kupandwa katika Shule ya Msingi Muungano iliyopo Kata ya Kiwalani Jiji la Dar es Saalam.

Akiongoza zoezi hilo la upandaji miti kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala Bi.Charangwa Selemani amesema “Kutokana na mabadiliko ya tabia ya Nchi inatupasa tupande miti kwa wingi ili kukabiliana na changamoto hii hivyo sisi kama Wilaya ya Ilala tumeweza kupanda miti elfu 11 na leo hii katika maadhimisho haya ya siku ya upandaji miti ngazi ya Wilaya tumeweza kupanda miti 300 katika Shule ya Msingi Muungano huku miti hiyo ikiwa ni miti ya matunda kama Miembe, Michungwa, Mipera, Mikungumanga pamoja na miti ya Kivuli hivyo nitoe wito kwa Waalimu na Wanafunzi kuhakikisha miti hii inatunzwa vizuri ili iweze kukua kwa wakati na tutakuja kukagua kuona kama mnatekeleza haya”.

Sambamba na hilo Bi.Charangwa ametoa wito kwa Wananchi wote kuhakikisha wanapanda miti kwa wingi katika maeneo yao ya makazi lengo likiwa ni kutunza mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi. “ Kulingana na kauli mbiu ya siku ya upandaji miti kitaifa isemayo ‘Miti ni Afya’ pamoja na kutekeleza maagizo ya Makamu wa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya kila Wilaya kuhakikisha wanapanda miti Milioni 1.5 kila Mwaka natoa wito kwa wananchi wote wa Wilaya ya Ilala kuhakikisha mnapanda miti kwenye makazi yenu ili tuweze kufikia lengo letu hivyo sisi kama Wilaya tutaendelea kushirikia na Wadau mbalimbali kuhakikisha tunapanda miti kwa Wingi hasa maeneo ya hifadhi ya mito pamoja na maeneo ya pembezoni mwa barabara”.

Akiongea kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Afisa Elimu Msingi Bi.Siporah Tenga ameeleza kuwa katika kutekeleza kampeni ya soma na Mti wanafunzi kila mwanzafunzi atatakiwa kupanda mti wake na kuhakikisha anautunza vyema, “Sisi kama viongozi tutahakikisha tunasimamia vyema zoezi hilo na kwa ukaribu zaidi kuhakikisha miti hii inayopandwa inatuzwa vyema na kuangaliwa kwa ukaribu zaidi ili iweze kukua kama ilivyotarajiwa.”

Naye Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa mazingira wa Halmasahuri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Theresia Denis ameeleza kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeendelea kutekeleza maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 ya kuendeleza programu mbalimbali za upandaji miti na ufugaji nyuki ili kutunza mazingira na kuongeza kipato kwa wananchi na Taifa.

Sambamba na hilo Bi.Theresia ameendelea kusema “Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeweza kushirikiana na Wananchi pamoja na wadau mbalimbali kubaini aina ya miti itakayopandwa na maeneo gani miti hiyo ipandwe ambapo katika kutekeleza hilo miti hiyo itaweza kupandwa maeneo ya hifadhi ya mto Msimbambazi, Msitu wa zingiziwa, maeneo ya Shule, zahanati pamoja na vituo vya afya pia zoezi hili linaenda sambamba na uhamasishaji wa wanafunzi kushiriki katika zoezi la upandaji miti ili kuwajengea tabia ya kutunza na kuhifadhi mazingira”.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Kata ya Kiwalani Bi. Christina Abraham Machenje ametoa shukurani zake za dhati kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Maliasili na auhifadhi wa Mazingira kwa kutuletea miti katika Shule ya Msingi Muungano kwani tunaahidi miti hii tutaitunza na itakua vyema hivyo nitoe wito kwa wananchi wenye mifugo ambayo huzurura maeneo ya Shule na kuharibu mazingira wahakikishe mifugo hiyo wanaifungia ndani lengo kuu ni kuhakikisha tunatunza mazingira ya Shule yetu kwa afya za watoto wetu.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.