• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

DC Ludigija aridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

Tarehe iliyowekwa: October 5th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Ngw'ilabuzu Ludigija  ameridhishwa na kasi ya miradi inayotekelezwa na kusimamiwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam huku akitoa  Maelekezo kwa viongozi wanaosimamia miradi hiyo, hayo yamebainishwa  katika muendelezo wa ziara yake aliyoifanya leo tarehe 05 Octoba,2022 ya kutembelea miradi ya maendeleo ikiwemo Ujenzi wa Vituo vya Afya na miundombinu mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Aidha miradi iliyoweza kutembelewa Katika  ziara hiyo ni pamoja na  ujenzi wa Soko la Kigogo Fresh, Ujenzi wa Kituo cha Afya Kinyerezi, Ujenzi wa Kituo cha Afya Segerea pamoja na shule ya Sekondari Liwiti  ambapo ujenzi wa soko la Kigogo Fresh lilogharimu takribani shillingi bilioni 2.6 ikiwa ni fedha za UVIKO- 19 linatarajiwa kukamilika ndani ya wiki tatu huku ujenzi wa kituo cha afya Kinyerezi kilichogharimu takribani kiasi cha shilingi milioni 500 ikiwa ni fedha kutoka mapato ya ndani na ujenzi uko asilimia 90  na hadi kufikia tarehe  30 Oktoba, 2022 ujenzi wa kituo hicho unategemea kukamilika pia ujenzi wa kituo cha afya Segerea pamoja na ujenzi wa shule ya Sekondari Liwiti ambayo inajegwa kwa fedha za mapato ya ndani pamoja na fedha za nje kutoka TAMISEMI takribani shilingi bilioni 1.4  hadi kukakamilika, jengo hilo lenye ghorofa tano linatarajia kukamilika hapo Desemba 2022 kwa ajili ya wanafunzi kuingia shule Januari 2023.

Akizungumza katika ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Ludigija ameelekeza kua ni afadhali kuchelewa kukamilisha miradi hiyo ya vituo vya afya lakini tujenge vituo bora na vyenye viwango vinavyotakiwa hivyo amewaelekeza Viongozi wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam  pamoja na wahandisi wanaosimamia miradi hiyo kuhakikisha inajengwa kwa viwango bora.

"Naelekeza kuwa wahandisi na wataalamu wetu wahakikishe wanadhibiti vifaa vinavyokuja kwenye  maeneo ya ujenzi ni vilivyokusudiwa na vyenye ubora kwani tusipofanya hivyo miradi mingi itakua inakwama na haendi kama ilivyokusudiwa hivyo tuhakikishe magari yote yanayoleta mchanga na kokoto hayamwagi kwanza hadi tupime iwapo tani wanazozisema zinaendana na mzigo walioubeba hivyo namuagiza Mhandisi wa Halmashauri kuhakikisha anatembelea maeneo yote yanayojengwa kwakutumia Force Account ili kuhakikisha vifaa vyote vipo sawa na utekelezaji unatekelezwa kwa kiwango bora." Ameelekeza Mhe. Ludigija.

Sambamba na hilo Mheshiwa Ludigija amempongeza Pindoria Construction Co. Ltd kwa kazi nzuri anayoifanya ya ujenzi wa shule ya sekondari Liwiti pia amemtaka aendelee na juhudi hizohizo ili hadi kufikia DIsemba 2022 mradi huo uweze kukamilika ili wanafunzi waweze kuanza masomo ifikapo Januari 2023

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.