• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la Dar es Salaam na jitihada za kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi

Tarehe iliyowekwa: October 5th, 2017

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita leo tarehe 05 Oktoba, 2017 amekutana na kufanya mazungumzo na ugeni kutoka Taasisi ya mtandao wa Majiji zaidi ya 90 duniani inayoshughulika na namna bora ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabia ya Nchi Duniani “C40 CITIES” ofisini kwake Karimjee jijini hapa.

Ugeni huo uliwakilishwa na Mkurugenzi wa C40 CITIES Kanda ya Afrika, Hastings Chikoko na Mkurugenzi C40 CITIES Kanda zote duniani kutoka jijini London, nchini Uingereza.

Akizungumza mara baada ya kufanya mazungumzo na ugeni huo, Meya Mwita amesema kuwa wamejadili mambo mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu yenye changamoto ya mafuriko, joto na usafiri jijini ili wananchi waweze kuepukana na athari za mabadiliko ya Tabia Nchi.

Amefafanua kuwa katika mazungumzo hayo Taasisi ya C40 imesema italeta mtalamu wa masuala ya Mabadiliko ya Tabia ya Nchi ambaye atafanya kazi kwa kushirikiana na wataalam wa Halmashauri za Jiji la Dar es Salaam ili kupata namna bora ya kushughulikia athari hizo jijini Dar es Salaam.

Amesema mbali na hilo lakini pia wameahidi kutoa fedha kwa ajili ya kukabiliana na athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi ikiwemo kuboresha maeneo ambayo yanakumbwa na mafuriko kama Bonde la Mto Msimbazi, Jangwani na maeneo mengine.

Meya Mwita aliendelea kueleza kwamba Jiji la Dar es Salaam limekuwa likikabiliwa na changamoto kubwa ya mafuriko kipindi cha mvua jambo ambalo husababisha baadhi ya wananchi kupoteza maisha, huku wengine wakikumbwa na uharibifu mkubwa wa mali zao.

“Mji wetu unakuwa kwa kasi kubwa, tunatakiwa kujipanga mapema, maeneo mengi yanakumbwa na mafuriko wakati wa mvua, wananchi wetu wanahangaika, sasa imefika kipindi ambacho tunapaswa kulipatia ufumbuzi jambo hili” amesema Meya Mwita.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa C40 CITIES Kanda ya Afrika, Hastings Chikoko ameeleza kuwa Jiji la Dar es Salaam lilijiunga na Taasisi ya C40 tokea mwaka 2014 na wamekua wakishirikiana pamoja na kubadilishana ujuzi na uzoefu namna bora ya kukabiliana na athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi hususani katika maeneo yanakumbwa na mafuriko, udhibiti wa taka ngumu na uboreshaji wa usafiri jijini.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa C40 CITIES, Simon Hansen alieleza kwamba lengo la mazungumzo yake na Mstahiki Meya wa Jiji ni kuwa na ushirikiano wa pamoja kati ya Jiji la Dar es Salaam na Taasisi ya C40 ili kuandaa Mpango Kazi wa namna bora ya kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi ikiwemo mafuriko, joto, ukame na Jiji la Dar es Salaam kama Majiji mengine duniani kuwa na mchango katika kupunguza ongezeko la joto duniani kutozidi 1.5 nyuzi joto kiwango ambacho kikifikiwa Athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi Duniani zitapungua.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.