• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la Dar lashika nafasi ya sita usafi wa Mazingira Afrika

Tarehe iliyowekwa: June 2nd, 2022

Jiji la Dar es Salaam limefanikiwa kuwa Jiji la sita kwa kuimarisha usafi wa mazingira ikilingwanishwa na miji mingine ya Afrika. Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Ng’wilabuzu Ludigija, amewaeleza wananchi kuhusu mafanikio hayo katika uzinduzi wa kampeni ya wiki ya mazingira duniani iliyoanza tarehe 02 Juni, 2022. Uzinduzi wa kampeni hiyo, ambayo kilele chake ni tarehe 05 Juni, 2022, umefanyika katika Kata ya Gerezani jijini Dar es Salaam.

 “Kwa hatua hiyo ya mafanikio, wadau wa mazingira mmelipatia heshima Jiji la Dar es Salaam kwa kulifanya kuwa mojawapo kati ya majiji masafi  barani Afrika kwa sababu kwa kutunza mazingira tunakuwa na afya bora na akili timamu inayotusaidia kutekeleza majukumu yetu vizuri, ” alisema Mhe. Ng’wilabuzu.

Mkuu huyo wa Wilaya aliwaelekeza wananchi kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya wiki ya mazingira isemayo “Tanzania moja tu. Tunza mazingira”, akisisitiza utunzaji wa mazingira uambatane na kazi ya upandaji wa miti ili kutimiza lengo la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam la kupanda miti milioni mbili na laki tano.

Mhe.Ludigija ameitumia fursa hiyo pia kuwapongeza wakandarasi wa usafi kwa kazi nzuri wanazozifanya kuimarisha usafi kupitia kampeni hiyo na kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi. Amewataka wakandarasi hao kuendelea na kazi zao bila kuchoka kwa kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ni taswira ya Tanzania kwa usafi.

Kwa upande wake, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Omari Kumbilamoto, amempongeza  Mkuu wa Idara ya Mazingira katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Rajabu Ngoda kwa kazi nzuri ya kuliweka Jiji safi kupitia Idara ya Mazingira.

Aidha, Mstahiki Meya amemuomba Mkuu wa Wilaya kuzifikisha salamu za wananchi wa Dar es Salaam kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwamba kwa takribani miaka sasa Jiji la Dar es Salaam halijawa na changamoto za magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu.

Katika uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Jumanne Shauri, naye aliwaambia wananchi kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imejipanga kufanya operesheni ya usafi kwa kuzingatia kwamba Jiji hilo ni kitovu cha shughuli nyingi. “Usafi unaanza na mimi. Timiza wajibu wako”, alisema Shauri akiahidi kuendeleza juhudi za kuimarisha usafi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.