• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Jiji la DSM kwa kushirikiana na C40 Cities kuweka Mikakati madhubuti ya Kuthibiti Taka Oza (Organic Waste)

Tarehe iliyowekwa: September 26th, 2024

Katika kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia Nchi yanayoambatana na athari za Kimazingira Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Kitengo cha  Maliasili na Uhifadhi wa Maziringira kwa kushirikiana na Umoja wa Majiji Duniani (C40 Cities) pamoja na wadau wa Mazingira kutoka Taasisi zisizo za Kiserikali wamefanya Warsha ya siku mbili yenye lengo la kukabiliana na  kuthibiti taka oza( Organic Waste) kwa Jiji la Dar es Salaam.

Warsha hiyo iliyoanza Septemba 25, na kuhitimishwa Septemba 26, imefanyika katika Hotel  ya Holiday Inn Jijini Dar es Salaam ikiwahusisha wataalamu wa mazingira kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam, wadau wa mazingira kutoka UK, AID na British High Commission pamoja na Taasisi zisizo za Kiserikali.

Akiongea wakati wa warsha hiyo Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Theresia Denis ameeleza kuwa kutokana na changamoto ya taka oza (Organic Waste) kushika hatamu hususani maeneo ya masoko, Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na C40 Cities pamoja na wadau wa mazingira wameweza kuanzisha mradi jumuishi wa mabadiliko ya tabia ya nchi uliotekelezwa katika Mtaa wa Butiama Kata ya Vingunguti, Bonyokwa pamoja na Shule ya Sekondari Zanaki ambapo taka hubadilishwa kuwa chakula cha kuku na mbolea pamoja na kusaidia kupunguza athari za kimazingira zinazotokana hizo.

Kwa upande wake Mshauri wa Jiji-mabadiliko ya tabia nchi Bw. Jophillene Bejumula ameeleza kuwa lengo la warsha hii ni kuendelea kuweka mipango madhubuti na ya muda mrefu  ya kuhakikisha hadi kufikia 2050 Jiji la Dar es Salaam lisizalishe hewa ya ukaa (Carbon) inayotokana na uzalishaji wa taka oza huku akitoa wito kwa wadau wengine wa mazingira kuendelea kutoa ushirikiano katika kutunza maingira kwa kuendelea kutenganisha taka ili kuepukana na magonjwa ya Mlipuko.

Naye Afisa Masoko Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bw. Alex Bubelwa amesema kuwa kutokana na warsha hiyo ni imani yake mradi wa kutenganisha taka oza utakua na manufaa makubwa katika kupunguza taka masokoni kwani taka za aina hizo huzlishwa  masokoni na kipindi cha mvua taka hizo ni changamoto katika utunzaji wa mazingira hivyo mradi huo utakua chachu ya kuweka mazingira katika hali ya usafi.

Aidha, Akieleza umuhimu wa Mradi wa jumuishi wa mabadiliko ya tabia ya nchi uliotekelezwa katika Mtaa wa Butiama Kata ya Vingunguti Jijini Dar es Salaam, Afisa Afya Mkuu wa Kata hiyo Bw. Geophrey Zenda ameeleza kuwa mradi huo umekua chachu ya uboreshaji wa mazingira pamoja na kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa sambamba na kupungua kwa magonjwa ya mlipuko kama Kipindupindu.

Akitoa Shukrani zake kwa wadau wa mazingira Mnufaika wa mradi jumuishi wa mabadiliko ya Tabia ya nchi Bw. Michael Humbi ambae ni mwenyekiti wa Kikundi cha wazalendo Butiama ameeleza kuwa mradi huo umeweza kuwapatia ajira kwani kupitia mradi huo wameweza kuzalisha mbolea ya Mboji na wadudu kwaajili yanchakula cha kuku ambavyo ni chachu ya wao kupata kipato pamoja na kuendelea kutunza mazingira.













Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.