• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

JMAT yafanya ziara ya kutembelea Soko la Kisasa la Nyamachoma "Kumbilamoto"

Tarehe iliyowekwa: May 22nd, 2025

Na: Doina Mwambagi

Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), chini ya Mwenyekiti wake Dr. Alhad Mussa Salum Leo tarehe 22 mei 2025, imefanya ziara ya kutembelea soko la kisasa la nyama choma la Kumbilamoto lililopo Vingunguti, kwa lengo la kujionea maendeleo ya mradi huo na kutambua mafanikio ya serikali katika kuboresha maisha ya wananchi.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa JMAT, Dr. Alhad amesema

“Tunashukuru kualikwa kutembelea mradi huu wa kimkakati na wa kombozi kwa wananchi. Maendeleo tuliyoyaona hapa yametufurahisha sana. Tumeridhika kuona kuwa wananchi wameondokana na adha walizokuwa wakizipata wakati wa jua kali na mvua. Tunatoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuweka mazingira bora ya kazi kwa watu wa kipato cha chini.”

Aidha, JMAT imesisitiza kuwa kusaidia kazi za mikono kwa wananchi ni njia madhubuti ya kuondoa umaskini na kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja, huku ikitoa wito kwa watanzania kuendeleza mshikamano na kumuomba Mungu aendelee kuilinda nchi kwa amani na utulivu ili kazi iendelee kufanyika kwa mafanikio.

Katika ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Mhe. Omary Kumbilamoto, ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya masoko huku akimpongeza Mkurugenzi wa Jiji hili Ndugu Elihuruma Mabelya, kwa kusimamia na kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa viwango vya kisasa.

Soko hilo la kisasa linategemea kuwa na zaidi ya wafanyabiashara 232, wakiwemo wauzaji wa nyama choma, mama lishe, wauzaji wa vinywaji, mbogamboga na viungo. Soko hilo linatarajiwa kuongeza mapato ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa wastani wa shilingi milioni 11 kila mwezi, ambayo ni zaidi ya shilingi milioni 100 kwa mwaka. Ujenzi wa soko hili umegharimu kiasi cha shilingi milioni 700.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Mstahiki Meya Kumbilamoto aongoza Madiwani kutembelea mradi wa kuzalisha na kuhifadhi maji wa Kidunda, Morogoro

    May 30, 2025
  • RC Chalamila atoa wiki mbili kwa wafanyabiashara kufungua njia zinazoelekea Soko la Kariakoo

    May 28, 2025
  • "Wakandarasi wanaokwamisha miradi ya maendeleo wasifumbiwe macho" - Waziri Mchengerwa

    May 24, 2025
  • "Kakusanyeni mapato bila kumuonea mtu" - Mkurugezni Mabelya

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.