• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Kata ya Kipunguni Halmashauri ya Jiji la DSM wafanya tamasha la maonyesho ya wajasiriamali ambao ni wanufaika wa Asilimia 10% ya mapato ya ndani

Tarehe iliyowekwa: January 27th, 2022

Na. Judith Damas

Uongozi wa Kata ya Kipunguni  kwa kushirikiana  na  Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii leo Januari 27, 2022 wameeandaa tamasha la maonyesho  ya wajasiriamali wa Kata ya Kipunguni yaliyofanyika  katika viwanja vya Moshi Bar Kata ya Kipunguni Jijini Dar es salaam lengo likiwa ni  kutambulisha bidhaa zao na kutoa elimu kwa wajasiriamali wanaofanya biashara na wanaotaka kuanzisha biashara zao ambapo  ni utekelezaji wa Sera ya Taifa ya uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya mwaka 2004.

Akiongea katika tamasha hilo mgeni rasmi ambaye ni Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Saady Khimji amesema "Kwa niaba ya Mstahiki Meya  Pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam napenda kuwahakikishia wananchi wajasiriamali wa Kata ya Kipunguni Kuwa tutashirikiana nanyi ili kuweza  Kuwawezesha wananchi wetu kujikwamua kiuchumi hususani wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. 

Aidha Mhe. Khimji amewapongeza Wajasiriamali wa Kata  ya Kipunguni  kwa kazi nzuri wanazozifanya hivyo amewaomba wajasiriamali  waliopata mkopo waweze kurudisha kwa wakati ili kuwapatia fursa wajasiriamali wengine kupata mkopo na kuendesha biashara zao.

Akitoa taarifa fupi ya vikundi vya Wanawake, vijana na watu wenye ulemavu Afisa maendeleo wa Kata ya Kipunguni Bi. Rozina Soka ameeleza kuwa Kata ya Kipunguni ni miongoni mwa Kata 36 za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambazo zimenufaika na mikopo ya asilimia 10% za mapato ya ndani inayolenga kuwawezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kuanzia mwaka 2019 hadi kufikia mwaka 2021.

Aidha Bi.Rozina  ameendelea kusema hadi kufikia Disemba 2021 Kata ya Kipunguni imeweza kusajili vikundi 46 ambavyo vimepokea mkopo wa shillingi milioni 432.5 ambapo vikundi  thelathink (30)  vya wanawake wamepokea shilingi milioni 217 huku vikundi kumi na nne (14) vya vijana vimepokea shilingi milioni 159.5 na vikundi viwili  (2) vya watu wenye ulemavu vimepokea jumla ya shilingi milioni 56. 

Sambamba na hilo Bi Rozina Soka amesema " Tunaishukuru Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kupitia Idara ya maendeleo ya jamii kwa kutuwezesha kupata mikopo japo kuna changamoto katika ufuatiliaji wa marejesho lakini sisi kama  viongozi tumeandaa mikakati ya ufuatiliaji  ngazi ya kata lengo likiwa ni kuhakikisha fedha zote za mkopo zinarejeshwa kwa wakati na vikundi vingine vinavyoomba mikopo viweze kupatiwa kwa wakati.

Vilevile shillingi milioni 598 inatarajiwa kutolewa kwa vikundi takribani arobaini na moja(41) ambavyo vishajadiliwa kwenye kikao cha kamati ya fedha na mara tu watakapokamilisha  taratibu zilizobaki watapatiwa mkopo huo.

Akitoa wito kwa wananchi   kwa niaba ya wajasiriamali wenzake wa Kata ya Kipunguni Bi. Mboni  Edd Gamuya amesema "Napenda kumshukuru Mkurugenzi wa Halmashauri wa Jiji la Dar es Salaam kwa kuona tija ya kutupatia mkopo  kwani mikopo hii imeweza kutukwamua kiuchumi na pia kwa kiasi kikubwa imeweza kutatua tatizo la ajira kwa vijana wengi.Pia ningependa kutoa wito kwawajasiriamali wenzangu ambao wanasuasua kurejesha mikopo yao warejeshe kwa wakati ili kuwapatia fursa wananchi wengine wanaoomba mikopo waweze kupata mikopo kwa wakati na kuweza kuendesha biashara zao.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.