• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Ludigija awaagiza watendaji kusimamia kwa umakini zoezi la urasimishaji ardhi

Tarehe iliyowekwa: June 6th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Ng’wilabuzu Ludigija, amewaagiza wenyeviti na watendaji wa mitaa katika Wilaya ya Ilala kushughulikia changamoto za urasimishaji ardhi katika maeneo ya kufuatia malalamiko ya wananchi dhidi ya makampuni yaliyopewa kazi ya urasimishaji ardhi kwa niaba ya Serikali.

“Nahitaji makampuni yote binafsi kusimamia urasimishaji wa ardhi kwa kushirikiana na kamati zilizoundwa na Serikali za Mitaa kuhakikisha jukumu la urasimishaji ardhi linakuwa na matokeo chanya ambayo yatatutoa katika changamoto za migogoro ya kila siku,” amesema Ludigija.

Mkuu huyo wa Wilaya amewaeelekeza watendaji wake kuendelea kutoa elimu ya ya kutosha  kwa wananchi kuhusu urasimishaji wa ardhi na faida zitokanazo na zoezi hili ili wananchi wawe na mwamko wa kuchangia kiasi cha fedha kilichopangwa na serikali.

 “Ombi langu kwa wenyeviti wote wa mitaa na watendaji wote ni kufanya vikao na wananchi wenu na kutoa elimu juu ya umuhimu wa urasimishaji ardhi kwa kutambua kwamba zoezi hili ni la kitaifa na kila mwananchi anapaswa kurasimisha sehemu yake,” amesema Ludigija.

Mhe. Ludigija amewaeleza watendaji hao kuwa zoezi hilo litasaidia kuimarisha usalama, kutoa fursa kwa wamiliki wa ardhi kupata na kunufaika na mikopo kutoka katika benki mbalimbali nchini. Aidha, ameyataka makampuni yote ya urasimishaji kuhakikisha wanakutana na kujadiliana kuhusu changamoto zinazosababisha baahi ya kampuni kushindwa kufanya kazi zao na kupotea na fedha za wanachi.

Kupitia fursa ya mkutano huo wa Mkuu wa Wilaya ambao ulihudhuriwa na wenyeviti na watendaji wa Serikali za Mitaa, wawakilishi wa makampuni ya urasimishaji ardhi na wadau mbalimbali katika sekta ya ardhi, mwakilisha wa Benki ya NMB, Irene Masaki ambaye ni Meneja Uhusiano kutoka katika kitengo cha huduma kwa wateja Kanda ya Dar es Salaam inayohusisha mikoa ya Pwani na Morogoro amesema kuwa benki ya NMB inafungua milango ya mikopo kwa wananchi kuwawezesha kupata fedha za kuchangia katika zoezi la urasimishaji.

Masaki amesema kuwa benki hiyo itatoa mikopo ya fedha kuanzia kiasi cha shilingi laki mbili hadi milioni moja ambacho taratibu zake za urejesha zina masharti nafuu ya kuwawezesha wananchi kurejesha kiasi kidogo cha fedha katika kipindi cha mwaka mmoja ili kuhakikisha suala hili la urasimishaji linafikia malengo.

Akiongea kwa niaba ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Tabu Shaibu, amesema Halmashauri ya Jiji itasimamia zoezi hilo katika kila kata kuweza kufikia malengo ya Serikali juu ya  urasimishaji wa ardhi nchini..

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.