• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mhe. Chande awataka Wananchi na Wafanyabiashara kuwajibika kulipa Kodi

Tarehe iliyowekwa: September 30th, 2023

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), amewataka watanzania kuwajibika kulipa kodi kwa kutoa na kudai risiti ya Mashine za Kieletroniki (EFD), ili kuhakikisha mapato ya nchi yanaongezeka na kusaidia kutekeleza miradi na huduma mbalimbali za kijamii.

Mhe. Chande, ametoa rai hiyo leo Septemba 30, 2023 wakati wa hafla kufunga wiki ya EFD iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato TRA wakishirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala yenye kauli mbiu isemayo ‘EFD, Risiti yako, Ulinzi wako, iliyokuwa ikifanyika viwanja vya Jakaya Youth Park Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo pamoja na wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama Machinga Mhe. Chande amesema “Nitoe wito kwa wafanyabiashara kushirikiana kikamilifu na mamlaka husika kutumia mashine hizi kwa usahihi ili kufanikisha adhma ya ulipaji kodi kwa maendeleo ya nchi yetu kwani kila mtanzania anapaswa kuwajibika katika kulipa kodi na kudai risiti halali ya kieletroniki kila anapofanya manunuzi lengo likiwa ni kuhakikisha tunazuia upotevu wa mapato hivyo niwaombe TRA kukusanya mapato halali bila usumbufu kwa wafanyabiashara”.

Aidha Mhe. Chande ameendelea kusema “Tuendelee kushirikiana kwa pamoja, na yule ambaye halipi kodi basi awe na utamaduni wa kulipa kodi kwa maslahi mapana ya Taifa letu na Serikali itawajibika kuleta maendeleo kwa wananchi wake, nanyi muwajibike kulinda na kuhifadhi miradi ya maendeleo inayoletwa na Serikali yenu”.

Naye Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Ndg. Alphayo Kidata ameeleza kuwa “Tumeandaa wiki hii ya EFD lengo likiwa ni kutoa elimu kwa Wafanyabiashara na Wananchi wote kwa ujumla juu ya matumizi sahihi ya EFD na kuhakikisha wanalipa kodi kwa wakati huku Wananchi wakihakikisha wanadai risiti kila wanaponunua bidhaa na Wafanyabiashara kutoa risiti kila wanapofanya malipo hivyo niwahimize muwe na utamaduni wa kutunza kumbukumbu zetu za EFD wakati mnapotoa risiti pia mfanye maisha yenu yawe ya kulipa kodi kwani kodi ni msingi wa maaendeleo ya nchi yetu”.

Hafla hii ya ufungaji wa Wiki ya EFD iliambatana na Sport Bonanza ambapo timu za wafanyabiashara, machinga pamoja na TRA Ilala na Kariakoo waliweza kushiriki michezo mbalimbali ikiwemo Mpira wa Miguu, kukimbia na vijiko, kuvuta Kamba, kukimbia na magunia pamoja na mchezo wa kuweka tenesi ndani ya bomba ambapo washindi wa michezo hiyo waliweza kupewa zawadi mbalimbali ikiwemo medali pamoja na Vikombe.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.