• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkurugenzi Jiji azungumza na Waandishi wa Habari maendeleo ya ujenzi Kituo Kikuu cha Mabasi Mbezi Luis

Tarehe iliyowekwa: November 7th, 2020

MKURUGENZI wa Halmashauri Jiji la Dar es Salaam, Bi. Sipora Liana amesema mradi wa Kituo Kikuu cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani katika eneo la Mbezi Luis umekamilika kwa asilimia 90 na unatarajia kuanza kutumika rasmi mwishoni mwa mwezi Novemba, 2020.

Liana ameyasema hayo leo tarehe 07 Novemba, 2020 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la mradi na kuwaeleza hali  halisi ya mradi ulipofikia ambapo amesema mradi huo upo katika hatua za mwisho za kukamilika kwake.

“Kama mnavyoona mradi umefikia hatua za mwisho na tarehe 30 ya mwezi huu utakuwa umekamilika kwa hatua ya kwanza kama ambavyo Mheshimiwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli aliagiza mradi huo uwe umekamilika hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Novemba” Amesema Liana.

Liana ameongeza kuwa kuanzia tarehe 25 ya mwezi huu mabasi yataanza kutumia Kituo cha Mabasi cha Mbezi Luis huku akiwataka wafanyabishara mbalimbali ambao wanataka kutumia fursa ya kufanya biashara katika Kituo hicho wajitokeza kufanya maombi.

Aidha, Liana amewataka wafanyabiashara ambao wanataka kufanya biashara katika Kituo hicho kuepuka matapeli ambao wanatumia mwanya huo kuwatapeli wafanyabiashara huku akiwasihi waombaji kufuata utaratibu ambao umewekwa wa kuomba kupitia mtandao kupitia anuani www.pangisha.tamisemi.go.tz kuanzia tarehe 09 Novemba, 2020.

Mkurugenzi Liana pia amezungumzia gharama halisi ya mradi huo kuwa ni shilingi za Kitanzania bilioni 50.9 ambazo zilitengwa hapo awali na kufafanua kwamba hakutakuwa na nyongeza ya fedha kwenye mradi huo.

“Nawaambieni mpaka sasa tumeweza kuokoa zaidi ya shilingi za Kitanzania bilioni 12 katika hizo bilioni 50.9 zilizotengwa kutokana na usimamizi dhabiti wa mradi huo kwa kuzingatia maelekezo ya Rais Magufuli katika kusimamia fedha za Serikali na sisi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam tumesimamia na kuweza kuokoa fedha hizi” Amesema Liana.

Liana ameendelea kueleza kwamba mradi huo ukikamilika utaweza kuingizia mapato Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam zaidi ya shilingi za Kitanzania bilioni 10 kwa mwaka.

Aidha, amesema Kituo Kikuu cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani katika eneo la Mbezi Luis kitaweza kutoa ajira kwa Watanzania zaidi ya elfu kumi na kuchochea uchumi kwa Watanzania na taifa kwa ujumla.

Mkurugenzi Liana amehitimisha kwa kueleza changamoto ya ucheleweshaji wa vifaa kulikotokana na mlipuko wa ugonjwa COVID-19 unaotokana na virusi vya CORONA na kupelekea makampuni ya nje kushindwa kuzalisha bidhaa kutokana na ugonjwa huo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.