• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa aagiza Machinjio kuanza kutumika

Tarehe iliyowekwa: July 8th, 2021

Na;Rosetha Gange

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe.Amosi makalla leo tarehe 8/7/2021 amefanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Machinjio ya kisasa ya Vingunguti na kutoa agizo kwa Mkandarasi wa machinjio hayo ambaye ni Shirika la nyumba la Taifa (NHC) kuwa, mpaka kufikia tarehe 30/7 ujenzi uwe umekamilika ili tarehe 1/8 ianze kutumika rasmi.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa Machinjio hayo Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Ndg.Jumanne Shauri amesema kuwa Halmashauri ya jiji la Dar es salaam ilisaini mkataba wa ujenzi wa Machinjio hayo na Shirika la nyumba la Taifa kwa gharama ya Sh.12.4Bil ambapo Sh.8.5 ni fedha kutoka Serikali kuu na Sh.3.9Bil ni mchango wa Halmashauri kutoka katika mapato yake ya ndani.

Aidha Ndg.Shauri amesema kwamba mpaka sasa Mkandarasi wa Machinjio hayo amekwishalipwa kiasi cha Sh.Bil 9 hivyo kubakiwa na deni la Sh.Bil.3.3.Mpaka sasa ujenzi wa Machinjio hayo umekwisha kamilika kwa 96% na wamejiwekea mpaka kufikia tarehe 1/8/2021 Machinjio hiyo ianze kutumika baada ya kukamilisha vitu vichache vilivyosalia kama ujenzi wa mabucha ya kuuzia nyama,kukamilisha ujenzi wa tanki la maji,kujenga banda la kuhifadhia ngozi pamoja na ujenzi wa chumba cha kuhifadhia baridi (cold room).

Akisisitiza kauli ya Kazi iendelee ya Mh.Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan,Mhe.Makalla amesema kuwa mradi wa machinjio hayo ni mkubwa na muhimu sana kwa nchi yetu hivyo ni lazima uanze kufanya kazi  haraka ili serikali iweze kujipatia mapato na matarajio yaliyolengwa na Serikali yaweze kutimia.

Mhe Makalla anasema,

“Mradi huu unakwenda kubadilisha maisha na uchumi wa watu.Pia ni mradi ambao unakwenda kufungua fursa nzuri kwa mikoa mingine kwa sababu Dar es salaam inategemewa sana katika soko la mifugo.Vilevile mradi huu utatoa fursa kwa wafanyabiashara kupeleka nyama maeneo mengine kama Zanzibar,Comoro na Dubai.Hivyo Mkandarasi fanya kazi usiku na mchana kukamilisha kazi iliyobaki.”   

Katika ziara ya ukaguzi wa Machinjio hayo Mhe.Makalla aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Ng’wilabuzu Ludigija,Meya wa Jiji la Dar es salaam Mhe.Omary Kumbilamoto,Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Ndg.Jumanne Shauri na watendaji mbalimbali kutoka Halmashauri ya jiji la Dar es salaam.

Mradi wa Machinjio ya kisasa ya Vingunguti ulianza rasmi tarehe 8 Julai 2019 ukiwa unatekelezwa na Mkandarasi ambaye ni Shirika la nyumba la Taifa (NHC) akisimamiwa na Mshauri Mwenezi M/S CONS AFRIKA Ltd na FB Consultant wa Dar es salaam.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.