• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam asikiliza kero za Wananchi wa Kata ya Zingiziwa

Tarehe iliyowekwa: November 20th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila leo tarehe 20 Novemba, 2023 amefanya mkutano wa hadhara wenye lengo la kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa Kata ya Zingiziwa ambapo ameahidi kuzipatia ufumbuzi kero mbalimbali zinazowakabili wananchi hao.

Katika mkutano huo RC Chalamila aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala , wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Viongozi wa Wilaya ya Ilala, Wataalamu kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na wengine kutoka Taasisi zinazowahudumia wananchi kwa ukaribu ikiwemo Wakala wa Barabara za Vijijini na Mji (TARURA) , Wataalamu kutoka Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira (DAWASA) pamoja na wataalamu kutoka Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO).

Akiwa katika kusikiliza kero za wananchi wa Kata ya Zingiziwa, RC Chalamila amepokea changamoto mbalimbali zikiwemo za Elimu, Miundombinu ya barabara, Maji, Umeme, Afya, migogoro mbalimbali ya Ardhi na changamoto za Kisheria ambapo zipo alizotatua papo kwa papo na nyingine kuzipatia utatuzi kwa kuwataka watendaji kuhakikisha wanazishughulikia Mara moja.

Hatahivyo, RC Chalamila amewataka viongozi wa TARURA katika Msimu huu wa mvua kurekebisha miundombinu ya barabara maeneo yenye uhitaji zaidi.

“Niwaombe Wataalamu kutoka TARURA na Halmashauri kuhakikisha msimu huu wa mvua mnrekebisha maeneo ambayo ni muhimu zaidi kwani tusije tukawa tunaweka fedha kwaajili ya kurekebisha miundombinu ya muda mfupi ila ikaharibika zaidi hivyo niwaombe wananchi muwe wavumilivu hadi mvua zitakapoisha ili miundombinu hiyo itengenezwe kwaajili ya matumizi ya muda mrefu”. ameeleza RC Chalamila

Sambamba na hilo RC Chalamila amesema suala la Usalama katika Mkoa wa Dar es Salaam limekua tishio hivyo itafanyika operesheni maalumu kwa baadhi ya maeneo ambayo ni ngome ya vikundi vya uhalifu maarafu kama 'Panya road' lengo likiwa ni kuhakikisha Dar es Salaam inakuwa katika hali ya usalama.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo ameeleza kuwa “Nitoe shukrani zangu kwako Mkuu wa Mkoa kwa kuona haja ya kuja kusikiliza kero za wananchi wa Zingiziwa hivyo nikuhakikishie tutazingatia haki katika kutekeleza yote uliyoagiza pia niwaombe wazazi kuwajibika kwani Serikali inatoa elimu bila malipo hivyo wazazi inabidi muwajibike kuhakikisha watoto wanakula, mkikaa kwenye vikao mkubaliane kupitia kamati zenu kuwa mtatoa kiasi gani kwaajili ya chakula cha watoto. Pia nipende kukuhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuwa tutahakikisha suala la ulinzi na usalama kwa wananchi wetu linachukuliwa hatua kwa wakati.”

Naye Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Tabu Shaibu amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa kutatua kero hizo kwa wakati “Tutahakikisha kero hizi tunazitatua kwa wakati bila kuathiri maeneo mengine kwani Wataalamu wetu tumewaelekeza kufuatilia maeneo yote yenye kero na kushughulikia kwa wakati hususani eneo la elimu, Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Jamii pamoja na eneo la sheria hivyo nipende kutoa shukrani zangu kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa ziara hii ya kutatua kero na nikuhakikishie tumejipanga kuondoa kero za wananchi wa Zingiziwa kwa ajili ya kukuza uchumi wao.”

Sambamba na hilo, ameeleza kuwa kwa upande wa Soko la Zingiziwa, shedi 5 za kisasa zinatarajiwa kujengwa ambapo ziko hatua ya usanifu na hadi kufikia Disemba 15 Shedi hizo zitakua zimekamilika.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.