• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ahimiza uzingatiaji wa lishe Bora kwa Mama wajawazito

Tarehe iliyowekwa: June 6th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amewataka mama wajawazito kuzingatia lishe bora kwani lishe bora wakati wa ujauzito ni muhimu sana kwa sababu humpatia mama virutubishi muhimu kulingana na hali yake. Wakati wa ujauzito mama anahitaji virutubishi zaidi kwa ajili ya maendeleo yake kiafya pamoja na mtoto aliyetumboni. Lishe bora huimarisha afya ya mama na humsaidia mtoto kukuwa vizuri kimwili na kiakili.

Mhe. Mpogolo ametoa wito huo leo Juni 6, 2024 wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uhamasishaji lishe bora kwa mama wajawazito na watoto wa umri chini ya miaka mitano katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar ee Salaam Sambamba na kauli mbiu isemayo ‘Lishe bora kwa baba, mama na mtoto ni msingi wa jamii bora na Taifa endelevu’.

Akiongea katika hafla hiyo Mhe. Mpogolo amesema “Taarifa zilizopo zinaonesha hali ya lishe miongoni mwa Watoto hairidhishi kutokana na kuathiriwa na tatizo la udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, uzito pungufu na ukondefu sasa tunapaswa kuchukua hatua stahiki kusimamia suala zima la watoto lakini pia Lishe bora kwa mama mjamzito hivyo nitoe wito kwa akina baba kushiriki katika kupambania masuala ya lishe kwa watoto wetu kwani Sisi kama Serikali tumeweka mikakati ya kuhakikisha wazazi na walezi wanazingatia lishe bora hii ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha jamii zetu zinazingatia afua za lishe hivyo zoezi hili linatarajiwa kufanyika kwa wiki moja ya kufanya tafakuri ya lishe ambayo ni lishe ya baba mama na mtoto”.

Sambamba na hilo, Mhe. Mpogolo Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha anazoendelea kuzitoa katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ya kuboresha miundombinu ya afya ili wananchi wapate huduma bora za Afya kwa wakati huku akieleza kuwa Serikali imeidhinisha shilingi bilioni 21 kwaajili ya ujenzi wa Hospitali tatu katika halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na tayari bilioni 15 zishawekwa na hospitali hizo zitaenda kujengwa eneo la Mnazi Mmoja kwa Jimbo la Ilala, eneo la Pugu kwa Jimbo la Ukonga na Segerea ambapo uwepo wa hospitali hizi utasaidia huduma za afya kupatikana kwa wakati.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Jiji la Dar es Salaam Dkt. Zaituni Hamza ameeleza kuwa Idara ya Afya, Lishe na Ustawi wa Jamii imeendelea kutekeleza maagizo ya kuhakikisha huduma za afya zinaboreshwa, lishe inazingatiwa pamoja na kupunguza vifo vya mama wajawazito kwani katika kutekeleza hayo Idara imekua ikifanya semina mbalimbali kuhusu lishe kwa mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano, huduma za mawasiliano zimeboreshwa kwani Idara imeweka namba ya dharura endapo mjamzito atapata changamoto atazitumia ili kupata huduma kwa uharaka hii itasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto pia katika hafla hiyo idara inaenda kuwapatia Kadi za CHIF watoto chini ya miaka mitano wanaoishi katika mazingira magumu hii inaonyesha ni jinsi gani idara inatekeleza maagizo ya kuboresha huduma za afya pamoja na kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya kwa wakati.

Aidha, katika Hafla hiyo kulikua na uzinduzi wa chanjo ya matone ya vitamini A pamoja na ugawaji wa mavazi ya uzazi (maternity Dress) kwa wamama wajawazito wasiopungua 100 na wanaonyonyesha zenye ujumbe usemao ‘asante mama Samia mimi na mtoto tuko salama’.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.