• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Awataka Wananchi Kupanda Miti Kwa Wingi

Tarehe iliyowekwa: March 29th, 2023

Katika kuelekea Siku ya Upandaji Miti ambayo hufanyika Kitaifa kila tarehe 01, Aprili, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Jonas Mpogolo leo Machi 29, 2023 amefanya kikao na waandishi wa habari lengo likiwa ni kuhabarisha, kuelimisha na kuhamasisha Umma juu ya upandaji wa miti hasa katika kipindi hichi cha mvua.

Akizungumza katika Kikao hicho Mhe. Mpogolo amesema ”Lengo la mkutano huu ni kuhabarisha, kuelimisha na kuhamasisha wananchi wa Wilaya ya Ilala kupanda miti kwa wingi hasa kipindi hichi cha mvua kwani kauli mbiu ya mwaka huu katika siku ya mazingira ni ‘Misitu ni Afya’ hivyo kutokana na kauli mbiu hii Inabidi tupande miti kwa wingi kwa afya na kwa kukuza uchumi pia, Sisi kama Wilaya tumedhamiria kupanda miti Takribani milioni 1.5 kama alivyoelekeza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philp Isdori Mpango mnamo Novemba 2022 akiwa Mbeya kuwa kila Halmashauri wahakikishe wanapanda miti takribani milioni 1.5 hivyo sisi tunatekeleza hilo ambapo kwa mwaka 2022 tuliweza kupanda takribani miti milioni 1.3 hivyo na mwaka 2023 tutahakikisha tunapanda miti milioni 1.5 katika baadhi ya maeneo yetu mabalimbali”.

Aidha Mhe. Mpogolo ameeleza kuwa kutokana na Kauli mbiu ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akishirikiana pamoja na Mkuu wa Mkoa ya ‘Mti wangu’ Wilaya ya Ilala watahamasisha zoezi la upandaji miti katika Shule za Msingi na Sekondari ambazo zina takribani wanafunzi laki 4 ambapo kila mwanafunzi akipanda mti wake zoezi hilo litakua limekamilika kwa kiasi kikubwa.

vilevile Mhe. Mpogolo amewataka viongozi wa Serikali za Mitaa na Kata kuhakikisha wanawahimiza wananchi wao kupanda miti kwa wingi huku akiwataka watu wenye majengo pembezoni mwa barabara pamoja na viwanda kuhakikisha wanapanda miti kwenye vungu na kuviweka mbele ya majengo yao ili kupendezesha mazingira na kuvutia mandhari ya Jiji letu la Dar es Salaam ambalo ndio kitovu cha wageni wengi wanapoingia Nchini Tanzania.

Sambamba na hilo Mhe. Mpogolo ameeleza kuwa kwa upande wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam itapanda miti ya matunda pamoja na miti ya kivuli hususani maeneo ya Mashuleni, pembezoni mwa barabara zetu na miti mingine itapandwa pembezoni mwa bonde la mto Msimbazi  "Kwa upande wetu Jiji la Dar es Salaam tutashirikiana na Wenzetu wa TFS kwani wameahidi kushirikiana na sisi katika kupendezeshanmazingira yetu hivyo wameahidi kutupatia miche ya miti mbalimbali inayoweza kupandwa katika Jiji letu.”

Aidha Mhe. Mpogolo ametoa wito kwa Wananchi kuhakikisha wanapanda miti kwa wingi kwani sheria ya saivi inamtaka mwananchi atenge asilimia 5 ya ardhi yake kuwa kijani hivyo ametaka Idara ya Mazingira ya Jiji la Dar es Salaam kuhakikisha wana kitalu cha miti kwani wataalamu wapo ambao watasaidiana nao kukamilisha jambo hilo la kupendezesha mazingira .

Kwa upande mwingine Mhe. Mpogolo alihitimisha kwa kuwataka wananchi kuchukua tahadhari kipindi hichi cha mvua hasa wanapovuka katika maeneo ya mito huku akitoa maagizo kwa Viongozi wa Serikali za Mitaa na Kata kuhakikisha wanachukua hatua za kisheria kwa wananchi wote wanaotiririsha maji taka wakati wa mvua hivyo kwa wananchi wote waliounganisha mfumo wa maji taka na mfumo wa maji ya mvua wahakikishe wanaacha tabia hiyo kwani wanachafua mazingira.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.