Barabara hii ya Magengeni Chang'ombe- African School iliyopo Tabata Jijini Dar es salaam ni moja ya Miradi saba (7) ya Maendeleo iliyopitiwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025 na kuwekwa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio hizo Bw.Ismail Ali Ussi.
Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 0.5 imejengwa kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji yatokanayo na Kodi za wananchi pamoja na tozo na ushuru mbalimbali ambapo jumla ya Shilingi milioni 678,978,390/= zimetumika mpaka kukamilika kwake.
Kukamilika kwa barabara hii kutasaidia kupunguza msongamano wa magari katika barabara za Tabata- Segerea na Baracuda-Chang'ombe.
Wana-Ilala wana kila sababu ya kumshukuru Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza kwa vitendo ahadi ya kuwatumikia Wananchi.
Barabara hii ya Magengeni Chang'ombe- African School iliyopo Tabata Jijini Dar es salaam ni moja ya Miradi saba (7) ya Maendeleo iliyopitiwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025 na kuwekwa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio hizo Bw.Ismail Ali Ussi.
Kukamilika kwa barabara hii kutasaidia kupunguza msongamano wa magari katika barabara za Tabata- Segerea na Baracuda-Chang'ombe.
"Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa 2025 Kwa Utulivu na Amani"
1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM
Anuani ya Posta: S.L.P 20950
Simu ya mezani: 0738 378 386
Namba ya Mkononi: 0738 378 386
Barua Pepe: info@dcc.go.tz
Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.