• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Omary Matulanga, Mstahiki Meya Jiji la Dar es Saaam, aahidi ushirikiano

Tarehe iliyowekwa: December 16th, 2020

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri za Manispaa za Jiji la Dar es Salaam leo tarehe 16 Desemba, 2020 katika ukumbi wa Karimjee wamemchagua Diwani wa Kata ya Tabata Mheshimiwa Omary Abdallah Matulanga kuwa Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam ndugu Paulo Mshimo Makanza, amesema uchaguzi wa Meya wa Jiji umehudhuriwa na Waheshimiwa Madiwani 140 kati ya 154 na kura zilizopigwa ni 140 ambapo kura za ndio zilikuwa 140 na hakukuwa na kura za hapana.

“Hivyo basi kwa mujibu wa Kanuni 13 (7) ya Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Tangazo la Serikali namba 417 la mwaka 2015 napenda kumtangaza ndugu Omary Abdallah Matulanga kuwa Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam”, Amesema Makanza.

Aidha, Makanza amefafanua kwamba Meya huyo mteule anatarajia kuapishwa Desemba 23 mwaka huu ambapo pamoja na mambo mengine utafanyika Mkutano wa kwanza wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, kuapishwa kwa Waheshimiwa Madiwani pamoja na Uchaguzi wa Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mstahiki Meya mteule Mheshimiwa Matulanga ametoa shukrani kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kumchagua kwenye nafasi hiyo huku pia akitoa pongezi kwa Waheshimiwa Madiwani wa Jiji la Dar es Salaam waliompigia kura za ndio na kumpa fursa ya kuongoza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

“Nina imani lengo letu kwa pamoja ni kuhakikisha Jiji hili linapiga hatua katika maendeleo na kuhakikisha tunafanikisha malengo ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli ya kuwaletea Watanzania maendeleo”, Amesema Matulanga.

Naye Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, ndugu Adam Ngalawa, amewataka Waheshimiwa Madiwani kuhakikisha wanasimamia kwa nguvu zote katika kutekeleza ilani ya chama hicho na kusisitiza kusiwe na migongano katika kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.