• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

RC Chalamila aipongeza Halmashauri ya Jiji la DSM kwa uboreshaji wa Mazingira katikati ya Mji

Tarehe iliyowekwa: May 29th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa uboreshaji wa mazingira katikati ya Mji lengo likiwa ni kuhakikisha Jiji la Dar es Salaam linakua safi sambamaba na madhari nzuri.

Mhe. Chalamila ametoa Pongezi hizo leo Mei 29, 2024 wakati akiendelea na ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Jiji la Dar es Salaam katika Jimbo la Ilala, ambapo aliweza kukagua maeneo manne ya Kata ya Kivukoni ikiwemo Ujenzi wa barabara ya Mindu,Mradi wa Perving mtaa wa Ohio na Karimjee pamoja na kukagua mradi wa uzibuaji mitaro eneo ya IT-Plaza.

Akiongea na wananchi na wafanyabiashara waliokuwepo maeneo hayo, Mhe. Chalamila ameeleza kuwa kutokana na mazingira ya Mjini kati kuwa katika hali  isiyo ridhisha, Jiji la Dar es Salaam limechukua hatua stahiki ya kuhakikisha mazingira ya Mji yanakua safi na mandhari ya Jiji inapendeza kwani Dar es Salaam ndio kitovu cha kupokea wageni na mikutano mingi ya Kimataifa inafanyikia katikati ya Miji hivyo uboreshaji wa mazingira hayo ni chachu ya kuvutia wageni katika Jiji la DSM.

“Nipende kuipongeza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa Hatua waliyoichukua ya kuboresha Jiji letu kwa kuweka perving na Kupanda miti na maua katika maeneo ya katikati ya Mji jambo linalofanya mandhari ya Jiji kuwa safi na kupendeza hivyo niwasisitize wafanyabiashara wote pamoja taasisi zote kutambua kuwa wajibu wao ni kuhakikisha Mji unakua safi pia napenda kuwapongeza Viongozi wa Jiji kwa kuchukua hatua ya kuzibua mitaro katika maeneo yaliyokua yanajaa maji wakati wa mvua kwani jitihada hizo zimepelekea kugundua kuwa kuna watu wanatiririsha maji machafu katika mifumo ya maji taka jambo ambalo linasababisha uchafu wa mazingira na kupelekea uwepo wa magonjwa ya milipuko, Sambamba na hilo nitaandaa kikao kazi kuzungumza na Watendaji wa Kata juu ya upendezeshaji wa Mji pamoja na kuongea na wadau na wamiliki wa majengo yote yalioko pembezoni mwa bararabara kutoka Airport hadi kufika Ikulu tuone namna gani tutapendezesha Jiji letu kwa kupanda miti pembezoni mwa barabara”.

Sambamba na hilo, Mhe. Chalamila amewataka PSSF pamoja na Ubalozi wa Canada kuhakisha ndani ya wiki moja wahakikishe wanatenganisha mfumo wa maji taka kwenye mfumo wa maji safi huku akiwataka wafanyabiashara wanaofanya biashara pembezoni mwa barabara katikati ya Mji waondoke na watafutiwe mahali sahihi pakufanya biashara zao ambapo wafanyabiashara wanaotambulika na sio kufanya biashara katika maeneo ya pembezoni mwa barabara ambayo ni mahususi kwaajili ya watembea kwa miguu.

Vilevile, Mhe. Chalamila ameweza kukagua ujenzi wa barabara ya Lindi ambapo amewaagiza Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Dar es Salaam( DAWASA) wahakikishe wanashughulikia tatizo la maji taka katika barabara ya Lindi ambayo yamekuwa kero kwa Wananchi wa Kata ya Ilala na wafanyabiashara wanaozunguka eneo hilo huku akiwataka Wakala wa Mabasi yaendayo Haraka (DART) kuhakikisha ndani ya wiki moja Mkandarasi anayetekelezaujenzi wa barabara ya Lindi anaanza ujenzi.

Awali akizungumza wakati wa Ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amesema “Baada ya kuona changamoto yaJiji la Dar es Salaam baadhi ya maeneo yanajaa maji wakati wa mvua tulichukua hatua stahiki za kuzibua mitaro maeneo ya Kamata, CBE pamoja na Muhimbili  ambapo tulibaini baadhi ya  majengo makubwa mifumo yao ya maji taka imeunganishwa kwenye mifumo ya maji safi, pia maeneo yote ya katikati ya mji yaliyowekwa pavings tunayatangaza kama Smart area na haturuhusu biashara yoyote kufanyika, hivyo nipende kukushukuru Mkuu wa Mkoa kwa ziara hii ndani ya Jimbo la Ilala kwani sisi kama Wilaya ya Ilala tutahakikisha mazingira ndani ya Jiji letu yanakua safi na tutaendelea kutekeleza yale yote uliyotuagiza lengo likiwa ni kuunga Mkono Juhudi za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kupendezesha Miji na kuwapanga wafanya biashara katika maeneo yao”.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo Cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Bi. Theresia Dennis ameeleza kuwa Jiji la Dar es Salaam liko katika kampeni ya uboreshaji wa mandhari katika maeneo yake ambapo shilingi bilioni 1.1 zimetumika kuboresha mandhari ya Jiji  katika maeneo 9 ya katikati ya Mji kuwekewa pavings pamoja na upandaji wa miti huku utekelezaji wa mradi huo ukiwa umekamilika kwa asilimia 95.












Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.