• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

RC Chalamila akagua miradi ya maendeleo ndani ya Jimbo la Ukonga

Tarehe iliyowekwa: May 28th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila leo Mei 28, 2024 amefanya ziara katika Jimbo la Ukonga ambapo amekagua miradi mitatu ikiwemo barabara ya Kitunda-Kivule-Msongola ,Hospitali ya Wilaya Kivule pamoja na ukaguzi wa tanki la maji lililopo Bangulo.

Akijibu maswali ya Wananchi wakati wa ukaguzi wa Barabara ya Kitunda-Kivule-Msingola, Mhe. Chalamila amesema Serikali inatambua changamoto ya Barabara hiyo ambayo imekuwa kero kwa Wananchi na kusema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe .Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia barabara hiyo iweze kujengewa kwa kiwango cha zege na utekelezaji kuanza Julai 2024.

Sambamba na hilo Mhe. Chalamila  amewataka Wananchi wa Kata ya Kivule pamoja na Kitunda  kuacha tabia ya kujenga mabondeni hali inayosababisha kujaa kwa maji katika makazi hayo na kuziba mitaro ya maji katika barabara.

"Kuna baadhi ya Wananchi wamekuwa na tabia ya kujenga kwenye maeneo ya barabara ambayo hupelekea njia za maji kuziba na hivyo mvua ikinyesha maji huingia barabarani, nipende kutoa rai yangi kwa Wananchi kuwa mara baada ya ukarabati, ujenzi utakapoanza kila mtanzania ajilinde mwenyewe kama amejenga eneo la barabara apishe ujenzi  na ikitokea mwananchi kukiuka hilo hatua stahiki zitachukuliwa”. Amesisitiza Mhe. Chalamila

Aidha Mhe. Chalamila pia aliweza kukagua ujenzi wa jengo la Wazazi katika Hospitali ya Wilaya Kivule ambapo aliwataka Wananchi kutumia miundombinu iliyopo huku akiwahakikishia kukamilika kwa miundombinu ya barabara kwani Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu ameboresha na anendelea kuboresha miundombinu ya afya ili kuendelea kuwasogezea wananchi huduma za afya kwa ukaribu zaidi.

Vilevile Mhe. Chalamila aliweza kukagua tanki la maji lililopo Bangulo ambapo aliwaeleza wananchi  adhma ya Serikali ni kuziondoa Changamoto zinazowakabili ikiwemo maji, umeme, urasimishaji na barabara ambapo amewahakikishia Serikali ni sikivu, kero zao zote zitaisha.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa ziara yake ya kukagua miradi pamoja na kuongea na wananchi katika maeneo yote aliyokagua huku akimuhakikishia kutekeleza yale yote aliyoyaagiza.

Naye Meneja wa Tarura Mkoa wa Dar es Salaam Eng. John Magoli ameeleza kuwa barabara ya Kitunda-Kivule kuelekea Msongola ina Kilometa 16 ambapo Mei 31, 2024 zabuni itafunguliwa na Julai 2024 ujenzi wa barabarara hiyo utaanza kutekelezwa kwa kiwango cha zege.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.