Na: Doina Mwambagi
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imetenga zaidi ya shilingi bilioni 18 kwa ajili ya kutoa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi 945 vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu katika mwaka huu wa fedha 2024/2025.
Akizungumza katika hafla ya utoaji wa mikopo isiyo na riba iliyofanyika leo tarehe 20 Juni 2025 katika viwanja vya Karimjee, Mkurugenzi wa Jiji hilo Ndugu Elihuruma Mabelya amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekuwa sauti na nguzo kubwa ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo isiyokuwa na riba inayotolewa na Halmashauri kwa mujibu wa sheria.
“Kazi kubwa tuliyonayo sasa ni kurahisisha utoaji wa mikopo hii na kuhakikisha hakuna changamoto kwa waombaji. Tumejipanga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna bora ya kuunda vikundi, kuomba mikopo, na kuhakikisha wanarejesha kwa ufanisi. Hatua hizi ni sehemu ya kuhakikisha tunatimiza dhamira ya Mheshimiwa Rais ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri,” amesisitiza Mabelya
Aidha, Mkurugenzi Mabelya amewatoa hofu wananchi kuhusu upatikanaji wa mikopo hiyo, akisisitiza kuwa fedha zipo na zitawafikia wanufaika wote waliokidhi vigezo, ili mikopo hiyo iweze kuchangia katika kuongeza kipato cha familia na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Mikopo hiyo itatolewa kupitia mfumo wa kibenki, ambapo Benki ya CRDB na Benki ya NMB zimepewa jukumu la kusimamia utoaji wa fedha kwa vikundi vilivyoidhinishwa. Mfumo huu unalenga kuhakikisha uwazi, usalama wa fedha, na ufuatiliaji mzuri wa urejeshaji wa mikopo.
1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM
Anuani ya Posta: S.L.P 20950
Simu ya mezani: 0738 378 386
Namba ya Mkononi: 0738 378 386
Barua Pepe: info@dcc.go.tz
Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.