• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Vivutio vya Utalii Dar vyawashangaza wanafunzi Chuo Kikuu cha New York

Tarehe iliyowekwa: June 7th, 2018

Ujumbe wa wanafunzi 15 kutoka Chuo Kikuu cha New York nchini Marekani wakiongozwa na walimu wao, Profesa Jens Rudbeck na Profesa Barbara Borst, wametembelea Jengo la kihistoria la Old Boma katika Jiji la Dar es Salaam tarehe 07 Juni, 2018 na kushangazwa na mambo mengi ya kuvutia waliyoyakuta katika jengo hilo nje ya matarajio yao.

Kati ya mambo yaliyowashangaza wanafunzi hao ni juhudi zilizofanywa na Serikali kupitia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuvionesha vivutio vyake vya utalii na uhifadhi wa majengo ya kihistoria katika Jiji hilo kwa kushirikiana na wadau kama vile Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage(DARCH) na Jumuiya ya Wabunifu Majengo Tanzania (Architect Association of Tanzania) ambapo matokeo yake halisi yameonekana kupitia jengo la Old Boma kwa ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya.

Katika jengo hilo ambalo ni Makumbusho ya Jiji la Dar es Salaam wanafunzi hao waliweza kupata historia yote ya Jiji la Dar es Salaam ikiwemo ya uhifadhi ya majengo na mambo ya kale na kujionea vivutio mbalimbali vya utalii katika jengo hilo ambalo linaendelea kuwa kivutio kikubwa cha utalii ndani na nje ya nchi. Hivi karibuni wanafunzi wapatao 35 kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam walifanya ziara ya kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii katika Jiji hilo likiwemo Jengo hilo la Old Boma.

Ziara ya wananfunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilikuwa ni ya kwanza kufanyika kwa madhumuni ya kukuza utalii wa ndani mara baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Suleiman Jafo(Mb) kuzindua rasmi shughuli za kukuza utalii katika Jiji hilo kupitia Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Miundombinu ya Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dar Rapid Transit), huduma za usafari zinazotolewa kupitia mradi huo na ukuwaji wa kasi wa Jiji la Dar es Salaam navyo vimekuwa ni sehemu ya vivutio vikubwa vya utalii kwa wanafunzi hao wa Chuo Kikuu cha New York.

Viongozi wa ujumbe huo, Profesa Rudbeck na Profesa Borst, kwa pamoja wameishukuru Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kufanikisha ziara yao na kuonesha nia ya kutembelea tena Dar es Salaam na wanafunzi wengine. Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Waziri Kombo, ametoa wito kwa ujumbe huo kuwa mabalozi wa Jiji la Dar es Salaam wa kuvitangaza vivutio vya utalii vya Jiji hilo katika sehemu mbalimbali nchini Marekani.

Ujumbe huo uliowasili nchini tarehe 04 Juni, mwaka huu unatarajiwa kurejea nchini Marekani tarehe 08 Juni, mwaka huu ukiwa umefurahishwa na maendeleo ya Jiji la Dar es Salaam, hususan juhudi zinazofanywa na Serikali kukabiliana na changamoto zinajitokeza katika eneo la mipango miji, ujenzi wa miundombinu ya barabara, maji, huduma za elimu na mpango wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wa kukuza utalii.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.