• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wanafunzi wa Olympio watembelea Strangnas

Tarehe iliyowekwa: May 30th, 2018

Wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi Olympio iliyopo Manispaa ya Ilala katika Jiji la Dar es Salaam, Johari Saleh na Anitha Masangula, wamepata fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu kwa siku saba na wanafunzi wenzao katika mji wa Strangnas nchini Sweden.

Johari, mwanafunzi wa darasa la sita na Anitha, mwanafunzi wa darasa la tano, wapo nchini Sweden kuanzia tarehe 25 Mei, mwaka huu kujifunza namna ya kutimiza wajibu wao kama wanafunzi kupitia mabaraza ya wanafunzi na mabaraza ya vijana kwa maslahi ya wanafunzi na vijana ikiwa ni sehemu ya wajibu wao katika ujenzi wa taifa.

Strangnas na Jiji la Dar es Salaam, kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Sweden(SIDA), wamekubaliana kuanzisha, kuboresha na kuimarisha mabaraza ya wanafunzi kama chombo kitakachowasaidia wanafunzi, chini ya ulezi wa walimu wao na Halmahauri zao za Manispaa, kutoa maoni yao kuhusu uboreshaji wa huduma na miundominu muhimu itakayochochea mafanikio yao katika elimu, kuwa viongozi bora na raia wenye uzalendo kwa nchi yao.

Nchini Sweden wanafunzi hao wanatembelea baadhi ya shule za msingi zenye mabaraza hayo na kubadilishana uzoefu na walimu na wanafunzi wenzao, kwa kuzingatia misingi ya demokrasia inayowapa uhuru wa kuwasilisha mawazo yao kama wanafunzi katika uongozi wa shule zao.

Johari na Anitha wameweza pia kukutana na baadhi ya viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Strangnas na kushiriki katika Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani wa Jiji hilo.

Shule za Msingi zilizomo katika mpango huo katika Manispaa ya Ilala ni Olympio, Zanaki na Kisutu.

Kwa uratibu wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Strangnas, Manispaa ya Ilala bado  ina fursa kubwa ya kuwawezesha wanafunzi wengine kujifunza nchini Sweden na wale wa Sweden kufanya ziara ya kujifunza nchini Tanzania.

Ufadhili wa SIDA kupitia mradi wake wa "Youth Democracy"  una lengo la kuimarisha mabaraza ya wanafunzi na vijana ili kuwaandaa kuanzia ngazi ya Shule ya Msingi kuelewa na kutekeleza wajibu wao katika taifa lao.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.