• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Wasimamizi wa Uchaguzi Jiji la DSM watakiwa kufuata maelekezo na sio kufanya kazi kwa mazoea

Tarehe iliyowekwa: October 1st, 2024

Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 katika Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Ndg. Elihuruma Mabelya amewataka wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi kufuata maelekezo na sio kufanya kazi kwa mazoea huku akisisitiza umuhimu wa kufuata taratibu na kanuni ili kuepusha sintofahamu zinazoweza kujitokeza katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika November 27,2024 Sambamba na kauli mbiu isemayo "Serikali za Mitaa sauti ya Wananchi jitokeze kushiriki Uchaguzi".

Wito huo umetolewa leo Oktoba Mosi, 2024 wakati wa ufunguzi wa semina ya mafunzo kwa wasimamizi wasaidizi kwa ngazi ya Jimbo, Kata na Mtaa uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Arnatoglou Jijini Dar es Salaam .

Aidha, Ndg. Mabelya ameeleza kuwa mafunzo hayo ya siku (1) yamelenga kuhakikisha kwamba uchaguzi unafanyika kwa haki na ufanisi, huku yakiwaandaa wasimamizi wasaidizi na kuwapa ujuzi wa kutosha katika kusimamia mchakato wa uchaguzi kwa kuhakikisha kwamba kila hatua inatekelezwa kwa mujibu wa sheria, Kanuni na taratibu za uchaguzi.

"Kwa mamlaka niliyopewa na kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya kifungu cha 201A cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka ya Miji) sura 288 kifungu cha 57(3) cha Sheria za Serikali za Mitaa pamoja na kanuni ya 7(1) ya uchaguzi wa viongozi wa mamlaka ya Serikali za Mitaa ngazi ya Vijiji, Vitongoji na Mitaa 2024 zilizotolewa kwa tangazo la Serikali namba 571,574 na 575 ya mwaka 2024 na Mwongozo wa Uchaguzi wa tarehe 09, Septemba  2024 vilivyotumika kwa ajili ya kuwateuwa kuwa Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa hivyo naamini baada ya mafunzo haya uchaguzi utafanyika kwa ufanisi mkubwa kwa kuzingatia sheria na kanuni za uchaguzi ili kuondoa malalamiko wakati wote wa uchaguzi."

Sambamba na hilo, Ndg.Mabelya amewataka washiriki hao kuzingatia mafunzo pamoja na kutoa uzoefu wao wa usimamizi wa siku za nyuma ili iwe rahisi katika utekelezaji wa jukumu zima la uchaguzi wa Serikali za Mitaa ifikapo Novemba 27, 2024 huku akiwakumbusha kuzingatia falsafa ya 4R (Reconciliation, Reform, Resilience na Rebuild) ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kifanikisha zoezi hilo kwa haki na uzalendo kwa maslahi ya Jiji na Nchi kwa ujumla.

Halikadhalika, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wamekula kiapo cha uaminifu, utii ,uadilifu na kutunza siri  katika kutimiza majukumu yao na kuwatendea haki watu wote kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.





Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.