• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Waziri Jafo atembelea eneo la ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi Mbezi Luis

Tarehe iliyowekwa: May 7th, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mheshiwa Selemani Jafo (Mb) leo tarehe 07 Mei, 2018 amefanya ziara ya kutembelea na kukagua eneo lenye hekari 12 ambalo Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatarajia kujenga Kituo Kikuu cha kisasa cha Mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani cha Mbezi Luis.

Akiongea mbele ya viongozi wa Mkoa na Jiji la Dar es Salaam Mheshimiwa Jafo amesema Serikali ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli imetoa fedha kiasi cha shilingi 146 bilioni kwa ajili ya miradi mkakati ya Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Jafo alieleza kwamba kati ya fedha hizo, shilingi 67.3 bilioni zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa stendi za mabasi 6 na stendi 2 za malori ambapo Jiji la Dar es Salaam limetengewa kiasi cha shilingi 50 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani cha Mbezi Luis.

Katika hatua nyingine Waziri Jafo amewataka viongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na busara wakati wa kutatua migogoro na ulipaji wa fidia kwa lengo la kuongeza eneo la ujenzi wa kituo hicho na pia kujenga miundombinu yenye ubora na inayozingatia mahitaji halisi ya wananchi hasa mamalishe, wamachinga na bodaboda na kuweza kukuza uchumi wa watu binafsi na taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Jafo alielekeza kwamba ujenzi wa Kituo Kikuu cha Mbezi Luis unapaswa uwe wa mfano kwa kuzingatia kuwa Dar es Salaam ni Jiji la biashara na ujenzi wa kituo hicho unategemewa kupunguza msongamano jijini na miundombinu yake inapaswa kuwa rafiki na kufikika kirahisi na watumiaji wa Kituo jirani cha daladala cha Mbezi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bi. Sipora Liana, alisema tathmini ya ulipaji wa fidia kwa wananchi imeshakamilika na hivi karibuni wananchi hao watalipwa stahiki zao na hadi tarehe 26 Juni, 2018 kazi ya ujenzi inatarajiwa kuanza baada ya Mkandarasi atakayeshinda zabuni kukabidhiwa eneo hilo la Mbezi Luis.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.