• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Waziri Mchengerwa awataka viongozi kusimamia vizuri na kulinda maslahi ya Walimu na Watumishi wote

Tarehe iliyowekwa: November 27th, 2023

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Mohammed Mchengerwa (Mb) amewataka viongozi wa Mikoa pamoja na Serikali za Mitaa kusimamia vizuri na kulinda maslahi ya Walimu na Watumishi wote Nchini wanaosimamiwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo leo wakati wa hafla ya kukabidhi vitendea kazi vipya ikiwemo Gari Toyota Coaster Mini Bus moja (1), Pikipiki 62 pamoja na Kompyuta mpakato 159 kwa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) iliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Tambaza Jijini Dar es Salam.

Akiongea wakati wa hafla hiyo Mhe. Mchengerwa ameeleza kuwa “Tunamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha sekta ya elimu nchini kwani zaidi ya shilingi bilioni 800 zimetumika kwaajili ya elimu bure hivyo kwa kutambua juhudi hizo inabidi tufanye kazi kwa bidii kwa kuhakikisha tunasimamia vyema miradi ya elimu ikamilike kwa wakati sambamba na kuhakikisha maslahi ya walimu yanazingatiwa na kulindwa kwani ili tutoe elimu bora lazima tutengeneze mazingira bora kwa walimu kwa kuzingatia misingi aliyotuachia Baba wa Taifa ya kuhakikisha tunapambana na adui watatu yani umaskini, maradhi na ujinga hivyo niwaagize TSC kufanya Mapitio kwa walimu wote wanaostahili kupanda vyeo ili waweze kupanda kwa wakati.”

Sambamba na hilo Mhe. Mchengerwa amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanasimamia miradi yote inayotekelezwa katika Halmashauri zao ikiwemo ujenzi wa madarasa kukamilika kwa wakati na ikitokea hawajakamilisha hatua za kisheria zitachukuliwa huku akiendelea kuwasisitiza Wakurugenzi wa Halmashauri kupanga mipango ya maendeleo inayoendana na matumizi husika ambayo yanalenga wananchi hivyo vipaumbele vya maendeleo viwaguse wananchi moja kwa moja.

Awali Akitoa  Shukrani zake kwa Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa  kuboresha sekta ya elimu nchini Mkuu wa Wilaya  Mhe. Edward Mpogolo amesema “Kwa kipindi cha miaka miwili ya Rais wetu Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam tumepokea zaidi ya bilioni 20 kwaajili ya kuboresha miundombinu ya elimu pamoja na kuendesha elimu bure ambapo nasisi kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri tumeweza kutengeneza madawati elfu 20 kwa Shule za Msingi pamoja na viti na meza 17,600 kwa shule za Sekondari za Halmashauri ya Jiji na utekelezaji unaendelea hivyo nikuhakikishie Mheshimiwa Waziri tutaendelea kusimamia yale yote utakayotuelekeza kwa maslahi ya Wananchi wetu na Nchi kwa ujumla.”

Kwa upande wake Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paulina Nkwama ameeleza kuwa shilingi milioni 454.6 fedha kutoka mradi wa boost zimetumika kununua vitendea kazi vilivyokabidhiwa kwa watendaji wa TSC nchini  ikiwemo  Pikipiki 62, gari moja kwaajili ya kazi za makao makuu, pamoja na kompyuta mpakato 159 ambapo 139 zitagawanywa katika wilaya zote Nchini huku 20 zikibaki kwa matumizi ya Makao makuu, hivyo kutoa shukrani zake kwa Rais na kumuhakikishia mpaka 2025 sekta ya elimu nchini itakuwa imeboreshwa zaidi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 0738 378 386

    Namba ya Mkononi: 0738 378 386

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.