• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Jiji
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha, Utawala na Utumishi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Udhibiti Taka
      • Mipangomiji, Mazingira na Usafirishaji
      • Afya na Huduma za Tiba
    • Vitengo
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Sheria na Usalama
      • Itifaki, Uhusiano na Umma
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Shughuli za Utalii
      • Dar es Salaam Yetu
      • Misitu na Mashamba ya wanyama wafugwao
      • Sehemu za kitamaduni, ngoma za asili na sanaa za mikono
      • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
      • Maeneo ya kupumzika, bustani na viwanja vya michezo
      • Maeneo ya Manunuzi
      • Majengo na maeneo ya kihistoria
      • Uwanda wa bahari, fukwe na visiwa
    • Urejelezaji wa Taka Ngumu
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Pikipiki
    • Vibali vya Maegesho ya Teksi
    • Vibali vya Kuingiza Magari ya Mizigo
    • Vituo Vikuu vya Mabasi
    • Udhibiti Taka Ngumu
    • Taarifa za Historia ya Viwanja
    • Mazishi ya miili ya marehemu wasiokuwa na ndugu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Uongozi
      • Kamati ya Mipangomiji, Mazingira na Miundombinu
      • Kamati ya Mipango na Ufuatiliaji
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
    • Mameya Wazamani wa Jiji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi iliyo kwenye Mpango
    • Miradi Inayoendelea
    • Vitega Uchumi vya Jiji
  • Machapisho
    • Sheria
    • Sheria Ndogo
    • Sera
    • Miongozo
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu za Maombi
    • Fomu za Ahadi ya Uadilifu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari Mpya
    • Matukio

Shirika la Masoko Kariakoo

Start Date: 1974-07-01
End Date: 1985-06-30

SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO (KARIAKOO MARKETS CORPORATION)


HISTORIA FUPI YA SOKO LA KARIAKOO


Historia ya jina Kariakoo na soko la Kariakoo inaanzia mwaka 1914 wakati nchi yetu Tanganyika ikitawaliwa na Wajerumani. Mahali palipo soko la Kariakoo palijengwa jengo na Wajerumani ambalo lilikua lifanywe ukumbi wa kuadhimishwa kutawazwa kwa mfalme Kaiser Wilheim wa Wajerumani lakini mara tu baada ya jengo kukamilika, vita kuu ya kwanza ilianza na Waingereza walipouteka mji huu wa Dar es Salaam walilitumia jengo hili kama kambi ya jeshi kwa askari walio julikana kama "Carrier corps” kwa jina la kigeni, yaani wabeba mizigo likitafsiriwa katika Kiswahili. Jina hilo la maaskari wabeba mizigo katika Kiswahili lilitamkwa kama “Karia-koo” na liliendelea kutumika kama jina la eneo lote linalozunguka mahali pale hii ndio historia ya jina Kariakoo.


Baada ya vita kuu ya kwanza kwisha, mwaka 1919 na nchi yetu kuanza kutawaliwa na Waingereza jengo hili  lilianza kutumika kama soko na kuanza kuhudumia wakazi  wa mji huu.
Wakati huo wafanya biashara walikua wakiuza bidhaa zao sakafuni kwa sababu hapakua na meza. Wafanyabiashara waliendelea kufanya biashara sakafuni hadi miaka ya 1960 wakati meza za saruji zilipo jengwa. Kwa kadri Jiji la Dar es Salaam lilivokua na wakazi wake kuongezeka, ndivyo kadri Soko hilo la zamani lilivyokua likishindwa kumudu kutoa huduma nzuri kwa wananchi. Pamoja na kubanana katika soko hilo na biashara kufanyika katika mazingira yasiyo ridhisha,  pia halikua na ghala za kutunzia vyakula wala vyumba vya barafu vya kuhifadhia vyakula.  Hali hiyo iliwafanya viongozi wa Halmashauri ya Jiji kuona haja ya kuwa na soko kubwa na la kisasa kulingana na maendeleo ya Jiji na hivyo wakaanza kujadili uwezekano wakujenga Soko jipya.


Uamuzi wakujenga soko kuu la Kariakoo la sasa, ulifanywa na Serikali mnamo mwaka 1970 baada ya majadiliano yaliyo chukua muda mrefu kati ya vyombo vya Serikali vilivyohusika. Serikali iliagiza Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kufanya mipango ya ujenzi wa soko jipya la kisasa ambalo lingechukua nafasi  ya soko la zamani lililokua hapa Kariakoo. Matarajio ya uamuzi huu wa Serikali wa kujenga Soko jipya yalikua ni kuwapatia wakazi wa Jiji mahala au Soko kubwa ambalo lingetosheleza mahitaji yao kwa muda wa miaka 50 hadi 70 ijayo kuhusu mambo yote ya vyakula, yaani uuzaji jumla, mahala pakuhifadhi vyakula na uuzaji wa rejareja. Mipango yote ilikamilika na ujenzi ulianza rasmi mwezi Machi, 1971. Ramani ya jengo la Soko ilitayarishwa na mchoraji wa ramani za majengo hayati Beda J. Amuli  ambaye ni mtanzania aliyeishi Dar es Salaam. Wajenzi waliojenga jengo la Soko ni Mwananchi Engeneering and Contracting Company (Mecco) wakisaidiana na makontrakta wengine kadhaa kwa kazi mbalimbali zilizo hitaji wataalamu maalumu. Shughuli zote za ujenzi zilimalizika mwezi Novemba 1975, na Soko lilifunguliwa rasmi kwa matumizi ya wananchi hapo tarehe 8 Desemba, 1975 na hayati Mwalimu Julius K.Nyerere, Raisi wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mpaka kukamilika, ujenzi wa Soko uligharimu jumla ya shilingi 22 milioni.


Soko la Kariakoo lipo kati kati ya eneo la Kariakoo katika kiwanja namba 32 zone 111 na limezungukwa na mitaa ya Nyamwezi, Mkunguni, Sikukuu na Tandamti.
Soko lina majengo mawili ambayo yameunganishwa katika ghorofa ya chini ya ardhi.  Majengo haya mawili pamoja na sehemu inayounganishwa yana eneo lenye jumla ya mita za mraba 17,780. Jengo la kwanza linaweza kuitwa Soko kubwa na jengo la pilli Soko dogo. Soko kubwa limegawanyika sehemu tatu ambazo ni ghorofa ya kwanza, ghorofa ya katikati, na ghorofa ya chini ambayo ni (basement). Soko dogo ni la rejareja ambalo ni tofauti sana na masoko mengine ya Dar es Salaam.



KUANZISHWA KWA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO 


1.0 UTANGULIZI


Shirika la masoko Kariakoo lilianzishwa kwa mujibu wa sheria ya Bunge Na.36 ya mwaka 1974. Mnamo mwaka 1985, sheria hiyo ilifanyiwa marekebisho kwa kurekebisha kifungu Namba 8 cha sheria hiyo. Katika marekebisho hayo Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam lilimilikishwa asilimia 51 ya hisa na Msajili wa Hazina akabaki na hisa asilimia 49. Sheria ya Shirika la masoko ya Kariakoo pia imefanyiwa marejeo mwaka 2002 (Revised edition) na kutambulika kama (The Kariakoo Makert Corporation revised Edition Act. No.132 of  2002 na kupewa majukumu yake makuu yafuatayo;

  • Kusimamia na kuendesha Soko Kuu la Kariakoo pamoja na Masoko mengine yatakayo kuwa chini ya usimamizi wa Shirika.
  • Kujenga Masoko mengine mapya katika Jiji la Dar es Salaam na kusimamia uendeshaji wake.

2.0 DIRA (VISION)

Dira ya Shirika ya Masoko ya Kariakoo kuwa Soko la kisasa katika Nchi za Afrika Mashariki na ya kati kwa kutoa huduma nzuri na endelevu hususani mazao ya vyakula,  pembejeo za kilimo na Bidhaa mchanganyiko zenye kujali Afya, mazingira na usalama wa watumiaji / walaji (consumers).

2.1 DHAMIRA  (MISSION)

Kutumia aina zote za rasilimali zilizopo na kuwashirikisha wadau mbalibmali katika kujenga uwezo endelevu na ushindani katika Soko la kibiashara linalikidhi haja za wadau, kudhibiti ubora wa bidhaa, mawasiliano na usafirishaji kwa ujumla .

2.2 TUNU ZA MSINGI (CORE VALUES)

Shirika la masoko Kariakoo linaamini yafuatayo katika utekelezaji wa shughuli zake

i.Hadhi na uwazi (Intergrity and transparency)

ii.Ushirikiano kazini (Teamwork)

iii.Kujituma na kuwajibika (commitment and accountability)

iv.Huduma bora (quality services)

v.Weledi (professionalism)

vi.Uwajibikaji kwa jamii (social responsibility)

3.0 UTAWALA/UONGOZI

Shirika la Masoko ya Kariakoo lipo chini ya Ofisi ya Raisi  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) Shirika lina wanahisa (2) ambao ni Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambayo ina HISA 51% na HAZINA  inayomiliki 49%.


MUUNDO WA SHIRIKA

(a) Bodi ya Wakurugenzi

Kwa mujibu wa sheria, Shirika linatakiwa kusimamiwa na Bodi ya Wakurugenzi. Ambapo Mwenyekiti wa Bodi huteuliwa na Mheshimiwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wajumbe wa Bodi huteuliwa na Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI).


(b) Menejimenti.

Chini ya Bodi iko Menejimenti inayoongozwa na Meneja Mkuu ambaye huteuliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano  wa Tanzania na ndiye Msimamizi Mkuu wa uendeshaji wa shuguli za kila siku za Shirika.

Shirika lina Idara nne (4) na Vitengo sita (6).

Soko la Kariakoo

Matangazo

  • Bajeti ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 June 14, 2023
  • Tangazo la Kuitwa Kwenye Usaili wa kuandika (Mtendaji wa Mtaa) September 19, 2023
  • Tangazo la Nafasi za Kazi za Mkataba October 20, 2023
  • TANGAZO DHIDI YA UTAPELI WA AJIRA July 20, 2022
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Waziri Mchengerwa awataka viongozi kusimamia vizuri na kulinda maslahi ya Walimu na Watumishi wote

    November 27, 2023
  • Uhusiano kati ya Jiji la DSM na Hamburg wazidi kuimarika

    November 27, 2023
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wahimizwa kupanda miti kwa wingi

    November 25, 2023
  • Waziri Mhagama awataka TARURA kuimarisha Kivuko cha Mwanagati-Magole

    November 22, 2023
  • Angalia zote

Video

NAPA
Video Zingine

Viunganishi vya Haraka

  • Mameya wa zamani wa Jiji
  • Vibali vya kuingia na Pikipiki katikati ya Jiji
  • Udhibiti wa Taka ngumu Jijini
  • Eneo Maalum la Usafi Jijini
  • Kituo cha Urithi wa Ubunifu Majengo na Utalii
  • Uwanda wa Bahari, Fukwe na Visiwa
  • Sehemu za Kitamaduni, Ngoma za Asili na Sanaa za Mikono
  • Majengo na Maeneo ya Kihistoria
  • Maeneo ya Kupumzika, Bustani na Viwanja vya Michezo

Viunganishi Linganifu

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • TAMISEMI
  • IDARA YA HABARI MAELEZO

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Anuani ya Posta: S.L.P 20950

    Simu ya mezani: 2128800

    Namba ya Mkononi:

    Barua Pepe: info@dcc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam. Haki Zote Zimehifadhiwa.