• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

DC Ilala amshukuru Rais Samia kwa fedha za ujenzi wa Soko la Kariakoo

Posted on: July 13th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Ng’wilabuzu Ludigija leo tarehe 13 Julai, 2022 amefanya ziara ya kukagua ukarabati na ujenzi wa Soko Kuu la Kariakoo, kwa lengo la kuona namna hatua za ujenzi huo unavyoendelea sambamba na matarajio ya kukamilika kwa mradi huo. Ukarabati wa soko hilo umetokana na ajali ya  moto iliyotokea miezi kadhaa iliyopita na kusababisha hasara kwa kuteketeza mali zilizopo.

Aidha, ukarabati huo unaenda sambamba na ujenzi wa Soko Dogo lililopo pembeni ya Soko Kuu la Kariakoo. Akiongea katika ziara hiyo Mhe. Ludigija amesema “Namshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha ambazo zinatumika katika ujenzi wa soko dogo na ukarabati wa soko kuu la kariakoo, shilingi Bilioni 28 Rais wetu amezitoa kukamilisha ujenzi huu, ikiwa Bilioni 26 kwa ajili ya Mkandarasi na Shiling Bilioni 2 kwa ajili ya Mshauri wa Ujenzi huu ambao ni Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), hii inaonesha namna Rais anajali wafanya biashara katika soko hili”.

Katika ziara hiyo Mhe. Ludigija aliambatana na wafanyabiashara pamoja na viongozi wa Soko Dogo na Soko Kubwa la Kariakoo na viongozi wa wamachinga kwa madhumuni ya kuja kuangalia ujenzi unavyoendelea na kuzidi kuwa na imani na Serikali juu wafanyabiashara wote kurejea pindi soko litakapomalizika.

“Napenda kuwahakikishia kwamba wafanyabiashara wote kuwa na usawa katika biashara kutokana na ukweli kwamba kuna wafanyabiashara wengi wamepisha ujenzi pamoja na ukarabati huu, hivyo basi wote muwe na subira na mtakuwa kipaumbele cha kwanza kurudi katika soko hili kama mwanzo ili mfanye biashara zenu bila ya wasiwasi”.

Sambamba na hilo, Mkuu wa Wilaya hiyo, alitoa wito kwa wafanyabiashara wadogowadogo maarufu kama Machinga kuacha mara moja kurudi katika maeneo ambayo siyo rasmi kwa wafanyabiashara na kuwasihii watengezaji wa simu za mkononi kutozuia Barabara za watembea kwa miguu.

Ujenzi na ukarabati wa soko kuu la Kariakoo mpaka sasa umefikia asilimia 28% ya ujenzi ikiwa unatarajiwa kumalizika mnamo Agosti, 2023 akieleza Mkandarasi wa Ujenzi huo Ndugu, Johnson Nyamwelu, amesema “katika nafasi yetu kama wakandarasi kwanza tunaunga mkono Serikali ya awamu ya Sita sambamba na kusimamia ujenzi huu ambao kwa sasa unaenda vizuri malengo yetu kumaliza kabla ya wakati ili kumheshimisha Rais wetu kwa utekelezaji bora wa ujenzi huu”

Ukarabati wa Soko Kuu la Kariakoo unatarajiwa kuboreshwa zaidi ukitofautisha na ulivyokuwa awali ikiwa maboresho zaidi katika kuongeza sehemu za biashara za mabenki, uwekwaji wa lifti, kuongeza maeneo zaidi ya wafanya biashara wadogo na wakubwa ikiwa ni dhamira ya kuweza kuwarudisha wote waliopisha ujenzi na ukarabati kurudi na kuendelea kufanya biashara kama awali.

Ziara hiyo ilihitimishwa kwa Mkuu wa Wilaya kuweza kutembelea Soko Kuu la Kisutu na kuweza kuongea na wafanyabiashara wa soko hilo ili kusikia kero zao pamoja na kutafuta njia ya upatikanaji wa suluhisho, sambamba na kuwsikiliza wafanya biashara katika soko dogo la Uuzaji wa Kuku.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.