• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

DSM-Hamburg Partnership wagawa Vifaa vya kujikinga na UVIKO 19 kwa Watoto wenye mahitaji Maalumu

Posted on: October 12th, 2021

Na: Rosetha Gange

Wakati wataalamu wa afya dunia wakiendelea kuumiza vichwa juu ya tiba ya kulimaliza kabisa janga la UVIKO 19, hapa kwetu Tanzania Serikali kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali zimekuwa zikiungana na wataalamu hao duniani kote katika kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kuhamasisha watu kupata chanjo, kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima, kuvaa barakoa wawapo kwenye mikusanyiko, kutumia vitakasa mikono na kunawa mikono kwa maji tiririka mara kwa mara.

Katika kuunga mkono jitihata zinazofanywa na Serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania,Shirika la Dar es salaam Hamburg Partnership linalomilikiwa na watu wa Ujerumani hapa Tanzania limegawa vifaa vya kujikinga dhidi ya maambukizi ya UVIKO 19 katika shule mbalimbali za watoto wenye mahitaji maalumu katika mkoa la Dar es salaam pamoja na kutoa elimu kwa watoto hao ya namna ya kutumia vifaa hivyo na njia nyingine za kujikinga na virusi vya Uviko 19.

Zoezi la ugawaji wa vifaa hivyo ulianza tarehe 4/10 na kumalizika 12/10/2021. Vifaa vilivyogawiwa ni Pamoja na stendi za chuma kwa ajili ya kuwekea ndoo za maji, ndoo za kutunzia maji na bomba zake, sabuni za maji za kunawia mikono pamoja na barakoa.

Akikabidhi vifaa hivyo Dr. Sylivia Ruambo ambaye ndiye Mratibu wa zoezi hilo amesema “Kama tunavyojua janga hili la UVIKO 19 lipo na tunapaswa kujikinga nalo sababu halichagui mtu mzima wala mlemavu.Tumeamua kuwasaidia Watoto wenye ulemavu kwa namna ya pekee kwa sababu changamoto wanazozipata wengine sababu ya ugonjwa huu na wao wanazipata lakini wao kutokana na hali walizonazo changamoto hizo huwa kubwa zaidi. Hivyo njia za kuwakinga kirahisi ni kuwawekea mashine za kunawia mikono karibu ili kuwarahisishia walimu na walezi wao waweze kuwasaidia kirahisi”  

Shule zilizokabidhiwa msaada wa vifaa hivyo ni Pamoja na Shule ya Sekondari Pugu, Shule ya msingi Mzambarauni, Shule ya msingi Buguruni Viziwi, shule ya Msingi Msimbazi Mseto,Shule ya sekondari Benjamini Mkapa,Shule ya msingi Uhuru mchanganyiko, Shule ya Sekondari ya wasichana Jangwani,Shule ya msingi Mtoni Maalumu, Shule ya msingi Sinza maalumu na Shule ya msingi Msasani.

Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dar es salaam, Afisa Elimu Maalumu wa Jiji Ndg.Swalehe Msechu ameishukuru Taasisi hiyo kwa kuwakumbuka watoto wenye changamoto mbalimbali kwani katika jamii mara nyingi kundi hili huwa linasahaulika sana. Hivyo kuwapa elimu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya UVIKO 19 kutawaepusha wao wenyewe na familia zao katika hatari ya kupata maradhi hayo.Pia ameahidi kusimamia utunzaji wa vifaa vyote vilivyokabidhiwa ili viweze kutumika katika matumizi sahihi yaliyokusudiwa.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.