• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam yapata hati safi, Meya Mwita aeleza siri ya mafanikio

Posted on: July 28th, 2017

Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepata hati safi kupitia taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali “CAG” kwa mwaka wa fedha 2015/2016.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa mara baada ya kumalizika kwa Kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kilichokuwa na ajenda moja ya kuwasilisha taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali “CAG", Mstahiki Meya Isaya Mwita alisema kuwa hati hiyo imetokana na kuwepo kwa usimamizi mzuri wa matumuzi ya fedha za Serikali.

Alifafanua kuwa kwa kiasi kikubwa tangu alipochaguliwa kushika nafasi hiyo, ameendelea kusimamia na kupunguza matumizi ya fedha ambayo hayakuwa ya lazima jambo ambalo limeleta heshima kubwa katika Halmashauri hiyo.

Aliongeza kuwa mbali na hiyo, lakini pia kwa kiasi kikubwa mapato ya Jiji yameongezeka kutokana na kusimamia kikamilifu vyanzo vya mapato yaliyopo ndani ya Jiji.

Alifafanua kuwa hati hiyo inaleta heshima kubwa ndani ya Jiji na kwamba imetoa nafasi kwa watendaji ndani ya Halmashauri kufanya kazi kwa umahiri zaidi ili kuweza kuleta maendeleo makubwa kwa wananchi. Alisema taarifa ya CAG imeeleza wazi kuwa hali ya utekelezaji ndani ya Jiji ni ya kuridhisha kutokana na usimamizi wa kutosha, kufuatilia mambo na hivyo kuweza kuyafanyia kazi mapendekezo ya ukaguzi wa miaka ya nyuma yaliyosalia.

"Baada ya kupata hati hii, sasa ni wakati mwingine Jiji kuendelea kufanya kazi za kuwatumikia wananchi ili waweze kunufaika na rasilimali zao, ukiangalia tumepewa dhamana kubwa ya kuwatumikia, hivyo kama Meya mwenye Jiji sina budi kuwatumikia wananchi kama inavyotakiwa” alisema Meya Mwita.

Aidha Meya Mwita alitoa wito kwa Halmashauri zilizopo ndani ya Jiji la Dar es Salaam kuwatumikia wananchi ikiwemo kutatua kero zinazo wakabili.

Wakati huo huo, Meya Mwita alisema kuwa Jiji limetenga Shilingi milioni 500 kwa ajili ya kununua maeneo ya makaburi kutokana na kuwepo kwa changamoto ya maeneo ya kuzikia watu. Alisema kwa sasa hali imekuwa mbaya kwenye maeneo ya Jiji na kwamba pesa hizo zitatumika kununua maeneo ambayo yatatumika kwa ajili ya kuzikia watu wanapopoteza maisha.

"Jambo hili litaanza kufanyika mwaka huu, kila Halmashauri itapatiwa eneo kwa ajili ya kuzikia watu, yapo maeneo ambayo tumepanga kuyanunua ukiangalia Jiji letu lina watu wengi sana, kadiri siku zinavyozidi kwenda ndivyo watu wanavyozidi kuongezeka. Leo hii imefikia hatua mtu ana zikwa juu ya mtu mwingine, jambo hili sio zuri” alisema Meya Mwita.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.