• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Jiji la Dar es Salaam na jitihada za kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi

Posted on: October 5th, 2017

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita leo tarehe 05 Oktoba, 2017 amekutana na kufanya mazungumzo na ugeni kutoka Taasisi ya mtandao wa Majiji zaidi ya 90 duniani inayoshughulika na namna bora ya kukabiliana na mabadiliko ya Tabia ya Nchi Duniani “C40 CITIES” ofisini kwake Karimjee jijini hapa.

Ugeni huo uliwakilishwa na Mkurugenzi wa C40 CITIES Kanda ya Afrika, Hastings Chikoko na Mkurugenzi C40 CITIES Kanda zote duniani kutoka jijini London, nchini Uingereza.

Akizungumza mara baada ya kufanya mazungumzo na ugeni huo, Meya Mwita amesema kuwa wamejadili mambo mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu yenye changamoto ya mafuriko, joto na usafiri jijini ili wananchi waweze kuepukana na athari za mabadiliko ya Tabia Nchi.

Amefafanua kuwa katika mazungumzo hayo Taasisi ya C40 imesema italeta mtalamu wa masuala ya Mabadiliko ya Tabia ya Nchi ambaye atafanya kazi kwa kushirikiana na wataalam wa Halmashauri za Jiji la Dar es Salaam ili kupata namna bora ya kushughulikia athari hizo jijini Dar es Salaam.

Amesema mbali na hilo lakini pia wameahidi kutoa fedha kwa ajili ya kukabiliana na athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi ikiwemo kuboresha maeneo ambayo yanakumbwa na mafuriko kama Bonde la Mto Msimbazi, Jangwani na maeneo mengine.

Meya Mwita aliendelea kueleza kwamba Jiji la Dar es Salaam limekuwa likikabiliwa na changamoto kubwa ya mafuriko kipindi cha mvua jambo ambalo husababisha baadhi ya wananchi kupoteza maisha, huku wengine wakikumbwa na uharibifu mkubwa wa mali zao.

“Mji wetu unakuwa kwa kasi kubwa, tunatakiwa kujipanga mapema, maeneo mengi yanakumbwa na mafuriko wakati wa mvua, wananchi wetu wanahangaika, sasa imefika kipindi ambacho tunapaswa kulipatia ufumbuzi jambo hili” amesema Meya Mwita.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa C40 CITIES Kanda ya Afrika, Hastings Chikoko ameeleza kuwa Jiji la Dar es Salaam lilijiunga na Taasisi ya C40 tokea mwaka 2014 na wamekua wakishirikiana pamoja na kubadilishana ujuzi na uzoefu namna bora ya kukabiliana na athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi hususani katika maeneo yanakumbwa na mafuriko, udhibiti wa taka ngumu na uboreshaji wa usafiri jijini.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa C40 CITIES, Simon Hansen alieleza kwamba lengo la mazungumzo yake na Mstahiki Meya wa Jiji ni kuwa na ushirikiano wa pamoja kati ya Jiji la Dar es Salaam na Taasisi ya C40 ili kuandaa Mpango Kazi wa namna bora ya kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi ikiwemo mafuriko, joto, ukame na Jiji la Dar es Salaam kama Majiji mengine duniani kuwa na mchango katika kupunguza ongezeko la joto duniani kutozidi 1.5 nyuzi joto kiwango ambacho kikifikiwa Athari za Mabadiliko ya Tabia Nchi Duniani zitapungua.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.