• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Jiji la DSM lapitisha Mpango na Bajeti ya Shilingi Bilioni 193.8 kwa mwaka wa fedha 2022/2023

Posted on: February 8th, 2022

Na: Hashim Jumbe

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo Tarehe 08 Februari, 2022 limefanya Mkutano Maalum wa Mapitio na Bajeti ya mwaka 2021/2022 kwa kipindi cha nusu mwaka (Julai-Desemba, 2021) na kufanya Makisio ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 wenye Jumla ya Shilingi Bilioni 193.8, ambapo kati ya fedha hizo Shilingi Bilioni 73.9 sawa na 38.1% ya Bajeti yote ni kutoka kwenye vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri na Shilingi Bilioni 119.9 sawa na 61.85% ya Bajeti ni fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu ambazo ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na Matumizi ya kawaida.

Aidha, kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Arnatouglou na kuongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto, kilipokea, kikajadili na kisha kupitisha Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo Bajeti ya Mapato ya ndani ya Halmashauri ya mwaka  wa fedha 2022/2023 imeongezeka kwa 16% ukilinganisha na Bajeti ya Shilingi Bilioni 62 ya mwaka 2021/2022, hii imetokana na mikakati bora iliyowekwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenye ukusanyaji wa mapato.

Katika kuandaa Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imezingatia Muongozo wa uandaaji wa Bajeti uliotolewa na Hazina Mwezi Februari, 2021, Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020, Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyoitoa Bungeni.

Sambamba na hayo, lakini pia uandaaji wa Mpango na Bajeti umezingatia Sheria ya Bajeti Na. 11 ya mwaka 2015 sura 439 pamoja na kanuni zake, Mkakati wa Taifa wa Mapambano dhidi ya rushwa, Malengo ya Mellania (SDGs 2030) Mpango Mkakati wa Halmashauri, Maoni ya wadau mbalimbali wa Halmashauri ambao wameshiriki katika maandalizi ya bajeti hii kuanzia ngazi ya Mtaa, Kata, Idara hadi Halmashauri kwa ujumla kwa kutumia mfumo wa Frursa na Vikwazo (O & OD iliyoboreshwa)

Aidha, katika makisio ya Mpango na Bajeti ya mwaka 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imejiwekea vipaumbele vyake pamoja na mikakati kumi na nne (14) itakayosaidia kufanikisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri ili iweze kutekeleza Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 kwa asilimia 100

Makisio ya Mapato ya Ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2022/2023

Akisoma taarifa kuhusu makisio ya mpango na bajeti ya mwaka 2022/2023 mbele ya Baraza la Madiwani, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Ndugu Jumanne Shauri, alisema "Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kukusanya  Shilingi Bilioni 73.9 kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani"

Matumizi ya Mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2022/2023

"Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kwenye Mapato yake ya Ndani inatarajia kutumia fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 73.9 katika mchanganuo ufuatao; Matumizi Mengineyo Shilingi Bilioni 22.04 sawa na 29.8% ya Bajeti, Mishahara Shilingi Bilioni 1.26 sawa na 1.7% ya Bajeti, Miradi ya Maendeleo Shilingi Bilioni 34.96 sawa na 47.26% ya Bajeti na Vyanzo Fungiwa Shilingi Bilioni 15.69 sawa na 21.21% ya Bajeti" Mkurugenzi Shauri

Makisio ya fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu

Ruzuku ya Shilingi Bilioni 119.9 kutoka Serikali Kuu imegawanywa katika maeneo mawili ambayo ni Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo

Mchanganuo wa Matumizi ya kawaida kwa fedha ya Ruzuku

"Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatarajia kutumia Shilingi Bilioni 98.15 ya fedha ya ruzuku sawa na 81.83% kulipa Mishahara na Shilingi Bilioni 2.628 sawa na 1.77% sawa na 1.47% kwa ajili ya Matumizi Mengineyo" alisema Shauri

Mchanganuo wa fedha za Miradi ya Maendeleo kwa fedha ya Ruzuku

Katika kipindi kijacho cha 2022/2023 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kutumia Shilingi Bilioni 19.99 kutekeleza Miradi ya Maendeleo ambayo ni sawa na 16.66%.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.