• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Jiji la DSM lapitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti ya Shilingi Bilioni 218.2 kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Posted on: February 10th, 2023

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo Tarehe 10 Februari, 2023limefanya Mkutano Maalum wa Mapitio ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2022/2023 kwa kipindi cha nusu mwaka (Julai-Desemba, 2022) na kufanya Makadirio ya Mpango na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 wenye Jumla ya Shilingi Bilioni 218.2, ambapo kati ya fedha hizo kiasi cha Shilingi Bilioni 90.7 sawa na 41.56% ya Bajeti yote ni makusanyo kutoka vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri na Shilingi Bilioni 127.5 sawa na 58.43% ya Bajeti ni fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu ambazo ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na Matumizi ya kawaida.

Aidha, kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Arnatouglou na kuongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe. Omary Kumbilamoto, kilipokea, kikajadili na kisha kupitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo Bajeti ya Mapato ya ndani ya Halmashauri imeongezeka kwa 10.7% ukilinganisha na Bajeti ya Shilingi Bilioni 80 ya mwaka 2022/2023, hii imetokana na mikakati bora iliyowekwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenye ukusanyaji wa mapato na uibuaji wa vyanzo vipya vya mapato. Katika Makadirio ya Mpango na Bajeti ya mwaka 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeweka Mikakati Saba (07) itakayosaidia kufanikisha ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri ili iweze kutekeleza Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 kwa asilimia 100, pamoja na kuwa na Vipaumbele Kumi (10) vya Mpango na Bajeti.

Makadirio ya Mapato ya Ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2023/2024

Akisoma taarifa kuhusu makadirio ya mpango na bajeti ya mwaka 2023/2024 mbele ya

Baraza la Madiwani, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Injinia Amani Mafuru alisema "Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kukusanya Shilingi Bilioni 90.7 kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani"


Matumizi ya Mapato ya ndani ya Halmashauri kwa mwaka 2022/2023

"Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kwenye Mapato yake ya Ndani inatarajia kutumia fedha kiasi cha Shilingi Bilioni 90.7 katika mchanganuo ufuatao; Matumizi Mengineyo Shilingi Bilioni 20.5 sawa na 22.6% ya Bajeti, Miradi ya Maendeleo Shilingi Bilioni 47.9 sawa na 52.8% ya Bajeti na Vyanzo Fungiwa Shilingi Bilioni 22.3 sawa na 24.5% ya Bajeti" alisema Injinia Mafuru

Makadirio ya fedha za Ruzuku kutoka Serikali Kuu

Ruzuku ya Shilingi Bilioni 127.5 kutoka Serikali Kuu imegawanywa katika maeneo mawili ambayo ni Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo

Mchanganuo wa Matumizi ya kawaida kwa fedha ya Ruzuku

"Kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inatarajia kutumia Shilingi Bilioni 107.3 ya fedha ya ruzuku sawa na 84.1% kulipa Mishahara na Shilingi Bilioni 1.36 sawa na 1.06% kwa ajili ya Matumizi Mengineyo" alisema Injinia Mafuru


Mchanganuo wa fedha za Miradi ya Maendeleo kwa fedha ya Ruzuku

Katika kipindi kijacho cha 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imepanga kutumia Shilingi Bilioni 18.6 kutekeleza Miradi ya Maendeleo ambayo ni sawa na 14.5%. Katika kuandaa Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imezingatia Mwongozo wa uandaaji wa Bajeti uliotolewa na Hazina Mwezi Desemba 2022, Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 hadi 2025, Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyoitoa Bungeni.

Sambamba na hayo, lakini pia uandaaji wa Rasimu ya Mpango na Bajeti umezingatia Sheria ya Bajeti Na. 11 ya mwaka 2015 sura 439 pamoja na kanuni zake, Mkakati wa Taifa wa Mapambano dhidi ya rushwa awamu ya Tatu, Malengo ya Maendeleo Endelevu, Mpango wa Mkakati wa Taifa wa kukuza uchumi na kupunguza umasikini Tanzania (MKUKUTA) II , Maoni ya wadau mbalimbali wa Halmashauri ambao wameshiriki katika maandalizi ya bajeti hii kuanzia ngazi ya Mtaa, Kata, Idara hadi Halmashauri kwa ujumla kwa kutumia mfumo wa Fursa na Vikwazo (O & OD iliyoboreshwa).

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la Msingi Kituo cha Afya Mzinga

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wakagua mradi wa vijana "Ulipo Tupo" Tabata

    June 03, 2025
  • Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Magengeni - Chang'ombe umewekewa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wazindua mradi wa Nishati Safi Soko la Samaki Feri

    June 03, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.