• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Kamati ya kudhibiti UKIMWI Jiji la DSM yatembelea vituo vinavyojishughulisha na uelimishaji wa shughuli za kudhibiti UKIMWI

Posted on: February 16th, 2022

Na: Judith Damas

Wajumbe wa kamati ya kudhibiti UKIMWI ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, leo tarehe 16 Februari 2022,  wamefanya ziara ya kukagua vituo  vinavyojishughulisha na utekelezaji wa kudhibiti UKIMWI vilivyopo Kata ya Buguruni Jijini Dar es Salaam .


Kamati hiyo inayoongozwa na Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam,  Mhe.Saady Khimji iliweza kutembelea vituo viwili vinavyojishughulisha katika kuimarisha Shughuli za kuthibiti UKIMWI ambovyo ni Kituo cha afya Buguruni ambacho kina kitengo cha huduma rafiki kwa vijana na Kamati ya kudhibiti UKIMWI Kata ambapo katika kituo cha afya Buguruni wameweza kupambana kudhibiti UKIMWI kwani wameweza kuanzisha huduma rafiki kwa vijana na pia wameweza kuanzisha kikundi cha Buguruni Youth Peer Educators (BUYOPE) ambacho hutumia sanaa mbalimbali kama ngoma pamoja na maigizo lengo likiwa ni kutoa elimu kwa vijana wengine juu Kujitambua na kujikinga  dhidi ya UKIMWI, ukatili wa kijinsia, elimu juu ya matumizi ya dawa za kulevya, elimu juu ya kutumia uzazi wa mpango pamoja na kujikinga dhidi ya magonjwa ya mlipuko ikiwemo ugonjwa wa Korona (COVID-19).


Akizungumza katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Saady Khimji ameweza kumpongeza Mganga Mfawidhi wa Kituo cha afya Buguruni pamoja na timu nzima ya madaktari na wauguzi kwa kuweza kuanzisha huduma rafiki kwa vijana kiafya na kijamii ambapo huduma hii itawaleta karibu vijana wetu hivyo kuongeza nguvu kazi ya Taifa letu.


Mhe. Khimji amesema "Nawapongeza sana vijana wa Buguruni Youth Peer Educators (BUYOPE) kwa shughuli mnazozifanya za kuelimisha Jamii juu ya kulinda afya zao pia kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuwaelimisha baadhi ya vijana wenye maambukizi ya UKIMWI lengo likiwa ni kuwasaidia, hivyo kwa vijana waliokwisha pata maambukizi ya virusi vya UKIMWI waweze kuunganishwa katika Konga ili kuweza kushirikiana na wengine katika kutekeleza shughuli za Konga."


Sambamba na hilo Mhe. Khimji ameeleza kua  kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam watahakikisha wanashirikiana na vikundi hivi kwa kuwawezesha vijana hawa kupata mkopo na pia watahakikisha kamati zote za kudhibiti UKIMWI ngazi ya Kata zina fanya kazi kikamilifu lengo likiwa ni      kuimarisha afya za wananchi hususani vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa na ambao ndio waathirika wakubwa wa majanga haya.


Naye Mratibu wa UKIMWI wa Halmashauri ya Jiji la DSM, Ndug. Barnabas Kisai ametoa shukrani zake kwa wajumbe wa Kamati ya UKIMWI ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaa na kuahidi ushirikiano katika kutekeleza yote aliyoagizwa kuyafanya ili kupunguza maambukizi ya usambaaji wa virusi vya UKIMWI na hatimaye kuongeza nguvu kazi ya Taifa.


Kwa upande wake Mratibu wa vijana Kituo cha afya Buguruni Sr. Janeth Nyera ameeleza kua huduma rafiki kwa vijana imeweza kuwa chachu kubwa kwa vijana kwani wameweza kuwaunganisha vijana wa makundi na rika mbalimbali wenye matatizo mbalimbali ya  kiafya na kijamii  ambao walikua na hofu ya kueleza matatizo yao kipindi cha nyuma hivyo kwa kushirikiana na vijana hao wameweza kuelimisha na kuwasaidia vijana wengi pia ameeleza kuwa vijana hao wameweza kutengewa siku yao maalumu ya kufika kituoni hapo ambayo ni siku ya Jumamosi hivyo ameahidi kushirikiana kikamilifu na Kamati ya kudhibiti UKIMWI ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam  na amemtaka mwakilishi wa Konga kuweza kuwatembelea kila Jumamosi ili kukutana na vijana walio na maambukizi ya VVU lengo likiwa ni kuwaunganisha na konga na kuwaelimisha zaidi ili wasikate tamaa ya maisha.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la Msingi Kituo cha Afya Mzinga

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wakagua mradi wa vijana "Ulipo Tupo" Tabata

    June 03, 2025
  • Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Magengeni - Chang'ombe umewekewa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wazindua mradi wa Nishati Safi Soko la Samaki Feri

    June 03, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.