• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Kamati ya Lishe yafanya Kikao cha kujadili taarifa za utekelezaji wa kazi za Lishe kwa Kipindi cha Robo ya Pili (Oktoba-Desemba 2023).

Posted on: March 15th, 2024

Kamati ya Lishe Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo Machi 15, 2024 imefanya Kikao cha kawaida cha Kujadili taarifa za utekelezaji wa kazi za Afya na lishe kwa kipindi cha Robo ya pili kuanzia Oktoba hadi Desemba 2023.

Akifungua kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Arnatoglou kwa niaba ya Mkurugenzi, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Tabu Shaibu amesema kuwa Halmashauri ya Jiji inatekeleza maagizo ya upatikanaji wa lishe kwa vitendo kwani Serikali ya Tanzania imedhamiria kuendelea kulipa umuhimu wa kipekee suala la lishe bora nchini ili kuhakikisha Tanzania inakuwa na uchumi imara kupitia maendeleo ya viwanda, hivyo elimu ya Lishe itasaidia uwepo wa watu (nguvu kazi) wenye afya njema ili kuwawezesha kufanya kazi kwa bidii na Kuchochea maendeleo ya nchi.

Katika kikao hicho Divisheni mbalimbali ziliwasiliisha taarifa za utekelezaji wa kazi za Afya na lishe kwa kipindi cha robo ya pili ambapo baada ya taarifa hizo Kamati iliweza kujadili na kutoa maelekezo kwa Divisheni ya Elimu Sekondari kuhamasisha zaidi suala la lishe kwa wanafunzi kwani inaonekana Shule nyingi za Sekondari wanafunzi hawapati mlo kamili.

Kwa upande wake Kaimu Mratibu wa Lishe wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Neema Mwakasege ameeleza kuwa Kamati imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa elimu ya lishe kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, wazazi na walezi na kuahidi kuendelea kutoa Elimu hiyo ikiwa ni sehemu ya kutekeleza dhamira ya Jiji la DSM ya kuhakikisha elimu inatolewa katika maeneo yote na watu wa rika zote.

Katika hatua nyingine, wajumbe wa Kamati Kuu ya Lishe waliweza kuchangia maoni Yao juu ya upatikanaji wa chakula mashuleni kwa kuwataka wazazi na walezi kuwa kipaumbele katika kuchangia ili watoto wasiweze kula vyakula ambavyo sio vya shule.

Katika upande wa Idara ya Mifugo imesisitiza ulaji wa nyama salama ambayo imepimwa vizuri nakuthibitishwa kwaajili ya kula.

Aidha, katika kikao hicho wajumbe walikubaliana katika kuongeza jitihada zaidi katika kuandaa programu za kuhamasisha na kutoa elimu za mara kwa mara kwa wananchi juu ya masuala ya lishe hususani mashuleni na kwa mama lishe ili kuboresha Afya za wananchi kwa maendeleo ya Nchi pamoja na kufanya ziara kutembelea mashule pamoja na viwanda ili kujionea kwa ukaribu utekelezaji wa shughuli za lishe.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • Mwenge wa Uhuru waweka jiwe la Msingi Kituo cha Afya Mzinga

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wakagua mradi wa vijana "Ulipo Tupo" Tabata

    June 03, 2025
  • Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Magengeni - Chang'ombe umewekewa jiwe la msingi na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa

    June 03, 2025
  • Mwenge wa Uhuru wazindua mradi wa Nishati Safi Soko la Samaki Feri

    June 03, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.