• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Siku ya Mazingira Duniani

Posted on: June 5th, 2017

Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wameungana na Wananchi wengine ulimwenguni kote katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani. Maadhimisho haya katika ngazi ya Mkoa yamefanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Siku ya Mazingira Duniani husheherekewa Ulimwenguni kote kila tarehe 5 Juni, kila mwaka. Madhumuni ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ni kuhamasisha jamii duniani kote kuelewa masuala yahusuyo Mazingira  na pia kuhamasisha watu wa jamii mbalimbali duniani kuwa mstari wa mbele katika kuchukua hatua za kuhifadhi na kulinda mazingira.

Awali, maadhimisho hayo yalitanguliwa na maandamano kutokea viwanja vya Posta ya zamani hadi viwanja vya Mnazi Mmoja na kupokelewa na mgeni rasmi Mhe. Sophia Mjema, Mkuu wa Wilaya ya Ilala ambaye alimuakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul C. Makonda.

Mhe. Sophia Mjema baada ya kupokea maandamano na utambulisho wa viongozi mbalimbali wa Serikali, wadau wa mazingira katika sekta binafsi na za umma alitoa shukrani za dhati kwa maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani na kupongeza juhudi za urejelezaji taka na kuwa mali zinazofanywa na wadau mbalimbali wa mazingira jijini Dar es Salaam.

Maadhimisho ya Siku ya Mazingira jijini Dar es Salaam yalianza tangu tarehe 31 Mei, 2017 na kufikia kilele tarehe 5 Juni, 2017 ambapo shughuli mbalimbali zinazohamasisha utunzaji wa mazingira katika maeneo mbalimbali zikiwemo:

  • Upandaji wa miti 10,747 kulikofanywa na Halmashauri za Manispaa za Jiji la Dar es Salaam katika maeneo ya wazi, maeneo ya mabondeni, mashuleni pamoja na maeneo ya pembezoni mwa barabara.
  • Usafi umefanyika kwenye maeneo ya mifereji, masoko na fukwe.

Mgeni rasmi aliendelea kueleza kwamba shughuli hizo ziliambatana na ukaguzi wa vifaa vya makampuni ya usafi na uhamasishaji kwa wananchi katika masula ya uhifadhi na usafishaji wa mazingira yanayowazunguka.

Mhe. Mjema ametoa wito kwa Wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kufahamu kwamba wao wana wajibu wa kuzuia madhara na mabadiliko hasi katika Mazingira na kuwaasa watendaji na viongozi wa Serikali waliopewa dhamana ya kusimamia sheria za kisekta na sheria ndogo za mazingira kuhamasisha jamii kufanya mazingira yao kuwa salama na masafi kwa lengo la ustawi wa maisha yetu na vizazi vyetu.

Akihitimisha hotuba yake, Mhe. Sophia Mjema amewaomba wananchi wote wa Jiji la Dar es Salaam kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ili kuifanya nchi yetu kuwa nchi ya viwanda, kuongeza mapambano dhidi ya dawa za kulevya, kuhimiza usafi wa mazingira na kuondoa utoroshaji wa raslimali katika nchi yetu.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Bi. Sipora Liana pia alipata fursa ya kutembelea banda la vijana wajasiriamali wanaorejeleza taka ngumu na kuwa bidhaa mbalimbali na kuwaeleza mpango wa Halmashauri ya Jiji wa kujenga miundombinu ya viwanda vidogo vidogo ili kuweza kuwafikishia huduma muhimu  vijana na wanawake kwa pamoja ili wajikwamue kiuchumi, kujiongeza kipato na kupunguza tatizo la ajira hasa kwa vijana na kina mama kwa kuwarasimisha wajasiriamali hawa wadogo ambao wengi hawako rasmi kwa kukosa sehemu za kufanyia kazi.

Kauli mbiu inayoongoza maadhimisho haya kimataifa ni “Connecting People to Nature”. Kwa Kiswahili ni: “Mahusiano Endelevu Kati ya Binadamu na Mazingira”. Kauli mbiu hii inahamasisha jamii kuwa na urafiki endelevu na mazingira asilia ambapo kila mtu anapaswa kutambua, kufurahi, kujivunia na kulinda uzuri wa mazingira asilia yetu na kuhamasishana kuyatunza na kuhifadhi.

Pamoja na kauli mbiu ya kimataifa, kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira mwaka huu kitaifa ni "Hifadhi ya Mazingira: Muhimili kwa Tanzania ya Viwanda.” Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka 2017 katika ngazi ya Taifa yanafanyika kijijini Butiama Mkoani Mara, ambako Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, alizaliwa, kukulia na kuzikwa. 

Madhumuni ya kupeleka maadhimisho haya Butiama ni kumuenzi Baba wa Taifa kwa sababu alikuwa mwanamazingira namba moja nchini mwetu lakini pia tunaenzi na kukumbuka mchango wake mkubwa katika masuala ya kuhifadhi mazingira nchini. Bila msimamo wa Mwalimu Nyerere kuhusu hifadhi ya mazingira, bila falsafa yake kuhusu uhifadhi, na bila hatua madhubuti alizochukua kulinda mazingira ya asili ya nchi yetu mapema kabisa tulipopata uhuru, nchi yetu isingekuwa inasifika kwa uzuri wake na vivutio vyake.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.