• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Mhe. Silaa Atoa siku saba kwa Maafisa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kutoa taarifa ya urasimishaji wa ardhi Mkoa wa DSM

Posted on: October 4th, 2023

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa (Mb) amewaelekeza Maafisa kutoka Wizara hiyo kuhakikisha wanafanyia kazi suala la urasimishaji wa Ardhi Mkoa wa Dar es Salaam kwani migogoro ya ardhi imekua mjadala mkubwa katika Mkoa huo.

Mhe. Silaa ametoa maelekezo hayo leo tarehe 04 Oktoba, 2023 wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam kujadili changamoto za ardhi zinazokabili Halmashauri tano za Mkoa wa Dar es Salaam.

Akizungumza katika Kikao hicho Mhe. Silaa amesema “Kazi kubwa ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma Muhimu kwa ukaribu zaidi hivyo ili kutimiza maono ya Rais wetu ni wajibu kuhakikisha tunapanga, tunapima na tunarasimisha ardhi kwa Wananchi wetu kama Ilani ya Chama inavyoelekeza hivyo niwahakikishie kutokana na kikao hichi changamoto zote za migogoro ya Ardhi katika Mkoa wetu zinaenda kupatiwa ufumbuzi na natoa siku Saba kwa maafisa kutoka wizara ya Ardhi kuniletea taarifa za urasimishaji wa Ardhi katika Mkoa wa Dar es Salaam ambapo kutokana na taarifa hiyo utekelezaji wa kukabiliana na migogoro ya ardhi kwenye Halmashauri zetu utaanza kuchukuliwa hatua stahiki.”

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Segerea Mhe. Bonnah Kamoli ameishukuru Kamati ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam kwa kuandaa kikao hichi chenye tija ya kutatua migogoro ya Ardhi kwa Wananchi huku akieleza kuwa suala la urasimishaji katika Jimbo la Segerea limekua changamoto hususani kata ya Kisukuru hivyo ameiomba Serikali kushirikiana na Wizara husika kutatua changamoto hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Mipango Miji na Mazingira  Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Nyansika Getama ambaye ni Diwani wa Kata ya Kivule ameeleza kuwa maeneo mengi ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam hayajafanyiwa urasimishaji jambo ambalo limekua likileta migogoro ya mipaka ya ardhi kwa Wananchi wa Jiji la Dar es Salaam hivyo ameiomba Wizara ya Ardhi kushirikiana na wataalamu kutoka Halmashauri ili kuweza kurasimisha maeneo hayo.

Awali akifungua kikao hicho Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam Ndg. Abasi Zuberi Mtemvu ameeleleza kuwa migogoro ya Ardhi katika Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam imekua janga kubwa kwani maeneo mengi ya Mkoa wa Dar es Salaam hayajapimwa wala kurasimishwa.

“Tumefanya Kikao hichi kwa Mara ya Kwanza na Waziri wa Ardhi kwani ndiye mwenye dhamana ya suala hili na kwakua tumejionea migogoro ya ardhi ikikabili Halmashauri zetu hii Ndio sababu ya kumualika Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwenye kikao hichi ili kuweza kusikiliza changamoto zote za ardhi za Mkoa wetu na kutupatia ufumbuzi juu ya changamoto hii.” Ameeleza Ndg. Mtemvu

Aidha kikao hicho cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam kiliweza kuhudhuriwa na Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa DSM, Makatibu Tawala, Wakurugenzi, Maafisa Ardhi kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Maafisa Ardhi kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.