• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaints |
Dar es Salaam City Council
Dar es Salaam City Council

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Dar es Salaam City Council

  • Home
  • About Us
    • City Profile
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Council Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Department
      • Finance, Administration and Personnel
      • Works and Fire Rescue
      • Waste Management
      • Urban Planning, Environment and Transportation
      • Health Services
    • Units
      • Planning, Monitoring and Statistics
      • Legal and Safety
      • Public Relations and Protocol
      • Internal Audit
      • Procurement and Supply
  • Investment Opportunity
    • Tourism Activities
      • Our Dar es Salaam
      • Animal zoos
      • Cultural Arts and Traditions
      • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
      • Public spaces, Garden and Sports
      • Shopping, Entertainment and Social life
      • Historical and Heritage building and sites
      • Beaches, Waterfronts and Islands
    • Recycling of Solid Waste
  • Our Services
    • Motorcycle Permit
    • Taxi Parking Permit
    • Car Parking
    • Bus Terminals
    • Solid Waste Management
    • Land History Information
    • Burial for unclaimed dead bodies
  • Councillors
    • All Councillors
    • Standing Committee
      • Finance and Administration Committee
      • Urban Planning, Environment and Infrastructure Commitee
      • Planning and Coordination Committee
      • Social Welfare Committee
      • Ethics Committee
    • Council Meetings
    • Lord Mayor's Timetable
    • Former City Mayors
  • Projects
    • Completed projects
    • Planned Projects
    • Ongoing Projects
    • City Investments
  • Publications
    • Acts
    • ByLaws
    • Policies
    • Guidelines
    • Reports
    • Application Form
    • Integrity Pledges Form
  • Media Centre
    • Press Release
    • Photo Gallery
    • Video Gallery
    • Speeches
    • News
    • Events

Mkuu wa Wilaya ya Ilala awataka Watendaji Kata kusimamia utekelezaji wa Afua za Lishe

Posted on: June 20th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amewataka Watendaji wa Kata kuhakikisha wanasimamia na kuhamasisha utekelezaji wa afua za lishe katika Wilaya hiyo ili kutokomeza udumavu na utapiamlo kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano.

Mhe. Mpogolo ametoa wito huo  leo Juni 20, 2024 wakati wa kikao cha kawaida cha Tathmini ya Mkataba wa lishe kilichofanyika ukumbi wa Arnatoglou Jijini Dar es Salaam  lengo likiwa ni kupitia viashiria vyote vilivyopo katika Mkataba wa lishe vilivyotekelezwa kwa robo ya tatu ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 (Januari-Machi 2024).

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mhe. Mpogolo amewataka wajumbe wa kikao hicho kufahamu kuwa lishe ndiyo msingi wa kila kitu katika jamii na kwamba kikao hicho ni muhimu sana katika uboreshaji wa lishe katika Jamii ili kuondokana na udumavu na utapiamlo kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano. “Napenda kuipongeza Idara ya Afya pamoja na watendaji wote kwa utekelezaji wa afua za lishe kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu lishe bora. Hivyo niwatake Watendaji wa Kata kuendelea kufanya vikao na kutoa elimu kuhusu lishe kwenye Kata zenu na kuweka maazimio kuhusu utekelezaji wa afua za lishe ili kufikia malengo”.

Sambamba na hilo, Mhe. Mpogolo Ameeleza kuwa ukosekanaji wa chakula kwa wanafunzi ni miongoni mwa sababu za udumavu na kuwasihi Watendaji wa Kata kuwaelimisha wazazi wajue umuhimu wa chakula shuleni kwa watoto  wao kwa kuhakikisha wanasimamia shule zote zinatoa chakula na wanafunzi wote wanapata chakula cha Mchana pindi wakiwa shuleni pamoja na kuhamasisha wazazi kutoa michango ya chakula kwa watoto wao sambamba na kufanya kampeni ya lishe bora kwa watoto huku akiwataka kufanya ziara mashuleni juu ya maadili, usalama, afya pamoja na masuala ya lishe kwa watoto ili waweze kuelewa masuala mbalimbali hususani masuala ya ukatili wa kijinsia ambayo yamekua yakiwakabili watoto wangi.

Awali akisoma taarifa ya tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa ngazi ya Wilaya, Mratibu wa Lishe Jiji la Dar es Salaam Bi. Flora Mgimba ameeleza kuwa viashiria vyote 11 vinavyopimwa katika utoaji wa huduma za lishe vimetekelezwa vizuri kwa kufikia hali nzuri ya utekelezaji kwani mafanikio yaliyopatikana kwenye utekelezaji kwa ngazi ya Kata ni kuimarika kwa ushirikiano kwa ngazi ya vituo, jamii na viongozi wa ngazi mbalimbali toka Wilaya hadi Mitaa pamoja na lishe kuwa suala mtambuka na kuongelewa katika ngazi mbalimbali za vikao katika jamii hasa kupitia watendaji na watoa huduma ngazi ya jamii huku akieleza mikakati ya kuboresha utekelezaji wa mkataba wa lishe katika ngazi mbalimbali ambapo Idara za Afya, Elimu Msingi na Sekondari pamoja na Watendaji wa Kata wameendelea kuhakikisha utekelezaji mzuri wa viashiria vyote vya lishe katika ngazi mbalimbali pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa lishe bora hususani kwa wanawake walio katika umri wa kuzaa na wajawazito.

Announcements

  • TAARIFA KWA UMMA February 19, 2025
  • TAARIFA KWA UMMA - MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA January 17, 2025
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2024 January 04, 2025
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2025 December 16, 2024
  • View All

Latest News

  • "Tutahakikisha tunasimamia Kata 36 na Mitaa 159 ili Jiji la DSM liwe safi" - DC Mpogolo

    May 03, 2025
  • Jiji La DSM laweka mikakati kushinda UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa

    April 29, 2025
  • Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waadhimisha Muungano kwa kupanda miti na kufanya usafi wa mazingira

    April 26, 2025
  • Zoezi la usafi wa mwisho wa wiki laendelea

    April 12, 2025
  • View All

Video

Msimbazi Basin Development Project Implementation Area
More Videos

Quick Links

  • Former City Council Mayors
  • Motorcycle's Permit
  • Solid Waste Management
  • Smart Area
  • Dar es Salaam Centre for Architectural Heritage
  • Beaches, Waterfronts and Islands
  • Cultural Arts and Traditions
  • Historical and Heritage building and sites
  • Public spaces, Garden and Sports

Related Links

  • BUNGE
  • Blogu ya Jiji
  • UTUMISHI
  • State House
  • Ilala Municipal Council
  • Tanzania Information Services

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    1 BARABARA YA MOROGORO 11882 DAR ES SALAAM

    Postal Address: S.L.P 20950

    Telephone: 0738 378 386

    Mobile: 0738 378 386

    Email: info@dcc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclaimer
    • Sitemap

Copyright © 2017 Dar es Salaam City Council . All rights reserved.